Mario Gomez alikuwa mapumzikoni ufukweni huko Forte dei Marmi akiwa na mke wake mwanamitindo Carina Wanzung
|
Mario
Gomez anafikiria kurejeshwa katika kikosi cha timu ya taifa ya Ujerumani baada ya kukosekana katika kikosi hicho kilicho ibuka na ushindi wa kombe la dunia kufuatia kusumbuliwa na majeraha ya muda mrefu.
Nyota huyu mwenye umri wa miaka 29 ameitumikia timu yake ya taifa kwa michezo 59 na kufunga magoli 25 huku mchezo wake wa mwisho kuonekana akiitumikia Ujerumani ni dhidi ya Paraguay ambapo walikwenda sare ya bao 3-3.
'Ni wazi mimi nataka kurejea katika timu ya taifa' Gomez kaliambia jarida la Bild
'Maandalizi yangu ya msimu wamekwenda vizuri na tunajiandaa vizuri kuanza msimu nchini Italia.'
No comments:
Post a Comment