Okwi akiwa karibu na mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba Zackaria Hans Poppe |
Kamati ya usajili ya klabu Simba imetangaza kumsajili mshambuliaji wao wa zamani Emmanuel Okwi ambaye msimu uliopita alikuwa kwa mahasimu wao wa soka Yanga.
Akiongea hii leo mwenyekiti wa kamati ya usajili ya klabu hiyo Zackaria Hans Poppe amesema wamemsajili Okwi baada ya mshambuliaji huyo raia wa Uganga kuomba kusajiliwa na klabu hiyo kufuatia kuvunjiwa mkataba na Yanga.
Poppe amesema mkataba wa Okwi na Simba ni wa wazi kwani mchezaji huyo ambaye amejiunga na Simba akiwa huru atakuwa huru kuondoka muda wowote atakapo taka kufanya hivyo.
Bofya Sauti ya Hans Poppe akiongea na waandishi wa habari kuhusu usajili wa Okwi
Kwa upande wake Okwi amewataka wapenzi wa Simba kumchukuliwa yeye kama mchezaji mpya kwao na kwamba wasahau yaliyopita na wampokee kama mchezaji kijana mpya kwao
Bofya sauti ya Okwi akiongelea usajili wake Simba
Kabla ya kujiunga na Yanga Okwi alikuwa akiichezea Sports Club Villa ya Uganda ambayo alijiunga nayo alitokea Etoile Du Sahel ya Tunisia ambako Okwi aliikimbia klabu hiyo kutokana na kile kilicho daiwa kuwa alinyimwa mshahara wake kwa zaidi ya miezi kinyume na makubalino ya mkataba.
Okwi anasajiliwa na Simba ikiwa siku mbili zimesalia kabla ya dirisha la usajili wa wachezaji wa ndani halijafungwa huku usajili wa wachezaji kutoka nje dirisha lake likitarajiwa kufungwa Septemba 6 2014
No comments:
Post a Comment