KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, August 29, 2014

YANGA YAMSHITAKI EMMANUEL OKWI TFF KWA KUSAJILIWA NA SIMBA

Mwenyekiti wa Yanga Yusufu Manji kulia na makamu wake Clementi Sanga wakitangaza kumshitaki Emmanuel OKwi ikiwa siku moja baada ya kusajiliwa na Simba hapo jana
Klabu ya Young Africans imemshitaki mchezaji Emmanuel Okwi kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na kuwasilisha nakala kwa shirikisho la soka Barani Afrika (CAF) na shirikisho la soka duniani (FIFA) kwa kuingia mkataba na timu nyingine wakati akiwa bado ana mkataba wa miaka miwili.
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Yanga mitaa ya Twiga/Jangwani, mwenyekiti wa Yanga Bw Yusuf Manji amesema wameshangazwa na kitendo hicho kilichofanywa na viongozi wa Simba , wakala wake na mchezaji mwenyewe.
"Emmanuel Okwi awali tulishapeleka malalamiko TFF na kuwapa nakala CAF na FIFA juu ya kufanya mazungumzo na timu ya Wadi Degla FC ya nchini Misri na kufikia klabu hiyo kutuma ofa ya kutaka kumnunua bila kuwasiliana na uongozi wetu" alisema Yusuf.
Ikiwa hilo tunasubiria majibu kutoka TFF jana mchezaji huyo amesaini mkataba mwingine, hii inaonyesha ni jinsi gani mchezaji huyu kuna watu walikua wanamrubuni,kwa kusaini mkataba mwingine kitu ambacho amekiuka sheria za FIFA za usajili.
Baada ya kuona jana amesaini mkataba na Simba, Yanga tulichokifanya leo ni kuandika barua nyingine TFF juu ya suala hilo na kuomba kulipwa fidia ya US Dollar 500,000  (sawa na TZS 800,000,000/=) kutoka kwa klabu ya Simba, wakala wake na mchezaji mwenyewe aliongeza "Manji"
Aidha uongozi wa Yanga umeiomba TFF kuwa imelipatia ufumbuzi suala hilo ndani ya siku saba, na kama siku saba zikikpita basi uongozi wa Yanga utakwenda moja kwa moja FIFA na ikishindakana mahakama ya soka CAS.
Lengo sio kuikomoa timu ya Simba, bali tunachotaka ni sheria ifuatwe, Okwi alikua ameitumikia klabu ya Ynaga kwa kipindi cha miezi sita tu, na kuwa amebakiza mkataba wa miaka miwili mpaka msimu mwishoni mwa msimu wa 2015/2016.
Mchezaji anayekutwa na kosa la kusaini sehem mbili adhabu yake ni kufungiwa kucheza soka kuanzia mwaka mmoja na kuendelea huku klabu husika ikifungiwa kusajili kuanzia miaka mwili na kuendela na kushushwa daraja au adhabu zote kwa pamoja.

No comments:

Post a Comment