KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, September 1, 2014

Manchester United yakamilisha usajili wa Daley Blind mtoto wa msaidizi wa Van Gaal katika timu ya taifa ya Uholanzi

Pichani ni Daley Blind aliyekamilisha uhamisho United
Ajax imethibitisha kuwa Daley Blind amejiunga na  Manchester United.

Vilabu hivyo vimefikia makubaliano kwa ajili ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 mwenye uwezo wa kucheza nafasi nyingi uwanjani wiki iliyopita ambapo United na Ajax walikubaliana ada ya uhamisho wake kufikia pauni milion £14.2 hii ikiwa ni baada ya mawindo ya muda mrefu ya mashitani wekundu.

Sasa imethibtishwa kua Blind atakuwa akiichezea United msimu huu baada ya kufanikiwa vipimo vya afya na kukubali maslahi ndani ya mshahara wake na kigogo hicho cha Premier League.

Blind ni mtoto wa nyota wa zamani wa timu ya taifa ya Uholanzi Danny, ambaye alikuwa ni msaidizi wa bosi wa United Louis van Gaal katika kikosi cha timu ya taifa ya Uholanzi katika michuano ya kombe la dunia na alianza kucheza soka kama mlinzi wa kushoto kabla ya kugeukia katika nafasi ya ulinzi wa kati katika klabu ya Ajax.

No comments:

Post a Comment