KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, September 17, 2014

Shirikisho la soka England kupunguza wachezaji nje ya jumuia ya Ulaya

Shirikisho la kandanda Uingereza, FA, limechapisha mpango unaonuia kupunguza wachezaji wasio wa asili ya muungano wa Ulaya (EU) wanaochezea taifa hilo kwa kiasi kinachoweza kufika asilimia 50. 

Watawala hao wa soka Uingereza wamechora orodha ya mabadiliko kwa muundo wa sasa katika harakati za kuongeza idadi na ubora wa talanta asili katika nchi hiyo. 

Orodha hiyo imewasilishwa kwa ligi ya Premier, ligi ya Kandanda na muungano wa wachezaji na mameneja na nia ya kuanza kuitekeleza kabla ya mwanzo wa musimu wa 2015-16. 

FA wanashikilia mpango huo utawezesha taifa lao kubobea kwenye Kombe la Dunia la 2022 nchini Qatar.

No comments:

Post a Comment