KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, October 13, 2014

Ander Herrera anasema United ni moto katika safu ya ushambuliaji

Wafumania nyavu wa United
Ander Herrera ameipongeza safu ya ushambuliaji ya Manchester United na kusisitiza kuwa klabu hiyo ina washambuliaji wakali zaidi duniani kwasasa.
Louis van Gaal alimsajili Radamel Falcao kwa mkopo wa muda mrefu katika siku ya mwisho ya usajili wa kiangazi ambapo mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Colombia akaungana na washambuliaji wengine wakali Robin van Persie na  Wayne Rooney ndani ya ngome kongwe Old Trafford.

Falcao aling'ara katika kushambulia goli katika kipindi chake cha uchezaji akiwa na Atletico Madrid na Monaco, na kupelekea Herrera kusema wazi kuwa Van Gaal, swali lililobaki kwasasa ni kwa kocha huyo kupanga mikakati ya kuimarisha uwezo wa ufungaji wa magoli katika msimu huu wa ligi kuu nchini England.
Amekaririwa Herrera akisema "I want to try to score more goals, It's very important for the midfielders.
Kisha akasema “I like assists as well and I think we have maybe the best three strikers in the world here in Rooney, van Persie and Falcao

No comments:

Post a Comment