KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, October 22, 2014

Dani Alves anakaribia kujiunga na Manchester United mwezi Januari

Manchester United wako katika maendeleo mazuri ya mazungumzo yao na mlinzi wa pembeni wa Barcelona Dani Alves wakati huu ambapo mlinzi huyo akiwa anakaribia kujiunga na Old Trafford.
United wamekuwa mbele zaidi katika mbio za kumuwania mlinzi huyo huku vilabu vingine kadhaa vya Premier League vikisukumwa na mpango wa kumsajili Alves wakiwemo Chelsea na Liverpool baada ya Alves mwenyewe kuitaka Barcelona kumruhusu kuondoka mwaka mpya.
Taarifa zinasema mpango huo unakaribia kukamilika ambapo mashetani wekundu wakiwa katika mazungumzo ya mwisho na Alves.
Tayari Mbrazil amejiweka tayati kuelekea Old Trafford na Louis van Gaal akipambana kukamilisha mpango huo.
Alves atatoa upinzani mkubwa kwa damu changa Rafael da Silva ndani ya kikosi cha United.

No comments:

Post a Comment