KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, October 30, 2014

David Silva huenda akaukosa mchezo dhidi ya United

Manchester City inasubiri kipimo cha mionzi cha mchezaji wake David Silva kujua kama nyota huyo wa kimataifa wa Hispania atakuwa fiti kuelekea mchezo wa mwishoni mwa juma wa 'derby' dhidi ya United.

Silva alitolewa baada ya dakika tisa katika mchezo dhidi ya Newcastle wa michuano ya League Cup ambao City walipoteza kwa bao 2-0 uwanja wa Etihad na tayari hofi ikitanda kuwa huenda akaukosa mchezo huo dhidi ya United.

Silva amefanyiwa kipimo hicho asubuhi ya leo katika viunga vya Etihad huku City wakitegemea majibu ndani ya saa 24.

Endapo majibu yatakuja kuwa yuko safi basi atalazimika kufanyiwa kipimo kingine cha afya Jumamosi kujua kama atakuwa na nafasi ya kucheza dhidi ya kikosi cha Louis van Gaal.

No comments:

Post a Comment