KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, June 28, 2012

Barcelona imekubali kutoa euro €14m kumsaini Alba

Jordi Alba

Barcelona imetangaza kupitia mtandao wa klabu hiyo imekubali kulipa ada ya kumsajili mchezaji wa Valencia Jordi Alba.
Kwa muda muda mrefu Barca maarufu kama Blaugrana imekuwa ikihusishwa kutaka huduma ya mlinzi huyo wa kushoto na sasa imebakia hatua ya mwisho ya kukamilisha usajili huo baada ya mazungumzo ya kina na kukubaliana kulipa ada ya uhamisho ya euro milioni €14.
Alba anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya wiki ijayo na kusaini mktaba wa miaka mitano endapo atafanikiwa kipimo hicho.
Taarifa kupitia mtandao wa klabu hiyo imesema
"Barcelona inatangaza kuwa leo tumefikia makubaliano na Valencia juu ya uhamisho wa Jordi Alba kilichobaki ni kipimo cha afya ambacho kitafanyika wiki ijayo" .
"gharama ya uhamisho wake ni euro milioni €14 na mchezaji huyo atasaini mkataba wa miaka mitano."

Alba ambaye kwasasa ana umri wa miaka 23, ni zao la Barcelona kupitia kituo chao cha kukuza vipaji “youth academy” lakini alishindwa kuingia katika kikosi cha kwanza Camp Nou na kuondoka mwaka 2005.
Sasa atakuwa akirejea nyumbani alikokulia baada ya kucheza klabu kadhaa kama Cornella, Gimnastic na Valencia.

No comments:

Post a Comment