KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, June 29, 2012

HABARI ZAIDI AJALI YA WAZIRI FENERA MUKANGARA

         Hali ya Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dokta FENELLA MUKANGARA aliyepata ajali leo asubuhi katika barabara ya Nzega-Shinyanga inaendelea Vizuri.
Msaidizi wa Waziri Ndugu JUMA MSADIKO ameiambia ROCKERSPORTS  kwa njia ya simu kuwa taratibu zinaendelea kufanywa ili kuangalia uwezekano wa kumpeleka Waziri huyo katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa ajili ya matibabu zaidi.
Amepata ajali ya gari katika Wilaya ya Nzega Mkoani Tabora akiwa njiani kwenda Mkoani Mwanza kikazi.
Habari kutoka Wilayani Nzega zinasema kwamba ajali hiyo imetokea wakati Waziri huyo akiwa njiani akitokea Dodoma kwenda Mkoani Mwanza kuzindua Mashindano ya Vishale.
 Kulingana na Msaidizi huyo wa Waziri, gari limepinduka mara Tatu wakati likilikwepa roli lilikokuwa mbele yao na Waziri huyo amepata majeraha kadhaa katika mwili wake.

No comments:

Post a Comment