KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, June 26, 2012

Ozil: Tutawafunga Italia nusu fainali

Mesut Ozil
Mesut Ozil anasema kuelekea katika mchezo wa nusu fainali Euro 2012 dhidi ya Italia wako sawa na watafanikiwa kutinga hatua ya fainali.
Italy imefanikiwa kutinga nusu fainali baada ya kuwachapa Waingereza kwa njia ya penati katika mchezo wa robio fainali uliopigwa jumapili iliyopita lakini kwasasa wanapimwa mbele ya Ujerumani wakionekana si lolote si chochote.
Licha ya Ujerumani kutokuwa na rikodi nzuri ya kuifunga Italia katika mashindano makubwa , Ozil anaamini kiu yao hiyo itafikia mwisho kule Warsaw siku ya alhamisi na kucheza fainali na ama Hispania au Ureno.
Ananukuliwa akisema
"mambo ya nyuma si kitu ,"anasema  Ozil .
Ameongeza
 "timu nyingine zinatuheshimu lengo letu ni kurejesha taji la Ulaya nchini Ujerumani tuko hapa kwa ajili hiyo. Tunaweza kuwafunga Italia.

No comments:

Post a Comment