Afisa habari wa TFF Bonface Wambura. |
Mzunguko
wa pili wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ambayo itatoa timu tatu
zitakazocheza Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao (2013/2014) unaanza
Jumamosi (Februari 2 mwaka huu) katika viwanja tisa tofauti.
Kundi
A litakuwa na mechi kati ya Mbeya City na Burkina Faso itakayochezwa
Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya, Majimaji na Kurugenzi katika Uwanja wa
Majimaji mjini Songea, na Polisi Iringa dhidi ya Mkamba Rangers kwenye
Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora mjini Iringa.
Mechi
za Kundi B, Jumamosi (Februari 2 mwaka huu) itakuwa Transit Camp na
Ndanda itakayochezwa Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani, Moro United dhidi
ya Villa Squad (Uwanja wa Karume, Dar es Salaam). Jumapili (Februari 3
mwaka huu) ni Tessema na Green Warriors (Mabatini, Pwani), Ashanti
United na Polisi Dar (Uwanja wa Karume, Dar es Salaam).
Kundi
C Jumamosi (Februari 2 mwaka huu) ni Polisi Dodoma na Kanembwa JKT
(Uwanja wa Jamhuri, Dodoma), Morani dhidi ya Mwadui (Uwanja wa Kiteto,
Manyara), Polisi Mara na Pamba (Uwanja wa Karume, Musoma), Polisi Tabora
na Rhino Rangers (Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora).
Ligi
hiyo inatarajiwa kumalizika mwishoni mwa Machi mwaka huu ambapo mshindi
wa kila kundi atapanda daraja kucheza Ligi Kuu msimu ujao. (Ratiba imeambatanishwa)
No comments:
Post a Comment