KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, August 3, 2013

Msimu mpya wa soka Ulaya kung'oa nanga

Wakati msimu mpya wa kandanda barani Ulaya unakaribia kuanza, nchini Ujerumani shughuli inaanza rasmi, kwa mechi za duru ya kwanza ya kombe la Shirikisho.

Michezo hizo linazishirikisha timu kutoka ligi kuu Bundesliga hadi za daraja ya sita, na kama kawaida matokeo ya kushangaza hayakosekani.

 Mechi 32 zinachezwa wikendi hii. Katika michezo ya mwaka jana, timu sita za Bundesliga ziliangushwa na timu za daraja za chini katika duru ya kwanza.

 Kila mtu atakuwa akisubiri kuona nani atachuana na nani, kuna yule atakayeweka historia na mashabiki wa soka wa Ujerumani watapata fursa ya kujua majina mengine kadhaa mapya katika kandanda.
 Fainali ya michuano hiyo kama kawaida huwa inaandaliwa katika uwanja wa Olimpiki mjini Berlin mwezi Mei.

 Matokeo ya leo




 


Germany: DFB Pokal


Finished
Magdeburg
Cottbus
(0-0)





Finished AET
TSG Neustrelitz
Freiburg
(0-0)





Finished
Wilhelmshaven
Borussia Dortmund
(0-0)





Finished
Bahlinger SC
Bochum
(0-2)





Finished
Fortuna Koln
Mainz 05
(1-1)





Finished
Lippstadt
Bayer Leverkusen
(1-3)





Finished
Neckarsulmer Sport Union
Kaiserslautern
(0-2)





Finished
SG Aumund-Vegesack
Hoffenheim
(0-0)





Finished
Sportfreunde Baumberg
Ingolstadt
(0-2)







 







 








Farasi wawili tena nchini Uhispania?
  Mchuano wa El Classico baina ya Barcelona na Real Madrid hutazamwa na mamilioni ya mashabiki kote ulimwenguni
Nchini Uhispania, bado zimesalia wiki mbili kabla ya ligi kuu ya La Liga kuanza, na tayari huenda ikawa rahisi kutabiri ni timu zipi zitamaliza katika nafasi ya kwanza na pili.

 Tangu mwaka wa 2008, Barcelona na Real Madrid zimekuwa zikimaliza katika nafasi mbili za kwanza, huku Barca ikishinda mataji manne ya ligi nayo Real moja katika misimu mitano iliyopita.

Kitu ambacho hakijulikani ni kama kocha mpya wa Real Carlo Ancelotti ataweza kubadilisha mambo, au kama kocha mpya wa Barca Gerardo Martino ataibakisha klabu hiyo kileleni.

 Vilabu hivyo viwili vimekuwa vikinufaika zaidi na fedha za haki ya matangazo ya televisheni kuliko vilabu vingine nchini Uhispania.
 
Barca na Real wawasajili nyota wapya
Wakati Barca wakiimarisha safu yao ya mashambulizi kwa kumsajili nyota wa Brazil Neymar, na wakati Real wakitarajiwa kuvunja rekodi ya uhamisho kwa kumsajili nyota wa Wales Gareth Bale, vilabu vingine vyote vimelazimika kuwa na wachezaji wao.

Atletico Madrid, ambao walimaliza wa tatu msimu uliopita na kisha wakawashinda Real katika fainali ya kombe la Mfalme, wamemmuuza mshambuliaji wao nyota Radamel Falcao kwenda AS Monaco. Real Soceidad ambao walimaliza wa nne wamemuuza kiungo Asier Illaramendi katika klabu ya Real wakati nambari tano Valencia wakimuuza nahodha Roberto Soldado katika klabu ya Tottenham Hotspur.

Kuondoka kwa Soldado kuna maana kuwa wafungaji mabao mengi katika La liga msimu uliopita, Falcao, Negredo na Soldado wote wamehama ligi hiyo.

 Pia mshambuliaji wa Uhispania Fernando Llorente ameihama Athletic Bilbao na kujiunga na Juventus. Hao ni wachache na kuna wengi ambao wamehama kutoka upande mmoja na kwenda upande mwingine.

Ratiba ya ligi ya Hispania mwezi huu itakuwa kama ifuatavyo.

Saturday, 17 August 2013
Real Sociedad v Getafe, 18:00
Valladolid v Athletic Bilbao, 20:00
Valencia v Malaga, 22:00

Sunday, 18 August 2013
Barcelona v Levante, 18:00
Osasuna v Granada, 20:00
Real Madrid v Real Betis, 20:00
Sevilla v Atletico Madrid, 22:00

Monday, 19 August 2013
Rayo Vallecano v Elche, 19:00
Almeria v Villarreal, 21:00
Celta de Vigo v Espanyol, 21:00

Friday, 23 August 2013
Getafe v Almeria, 19:00
Athletic Bilbao v Osasuna, 21:00

Saturday, 24 August 2013
Elche v Real Sociedad, 18:00
Espanyol v Valencia, 20:00
Villarreal v Valladolid, 22:00

Sunday, 25 August 2013
Atletico Madrid v Rayo Vallecano, 18:00
Levante v Sevilla, 20:00
Malaga v Barcelona, 20:00
Real Betis v Celta de Vigo, 22:00

Monday, 26 August 2013
Granada v Real Madrid, 20:00

No comments:

Post a Comment