KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, December 26, 2013

Wakati United ikiishinda Hull City 3-2 katika benchi la ufundi David Moyes alikuwa nyuma ya Sir Alex Furguson

Alex Ferguson akipeana mikono na mashabiki wakati akichukua kiti karibu na sehemu ya makocha wa United pembeni yake ni Wilfried Zaha (kushoto)
Meneja wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson anaonekana kuendelea kuwepo karibu sana na ratiba za michezo ya klabu hiyo, ambapo hii leo ikiwa ni siku ya kufunguza zawadi za sikukuu ya Krismass yaani 'Boxing Day' akionekana dimbani katika mchezo wa klabu hiyo dhidi ya Hull City uliopigwa KC Stadium.
Fergie ameonekana akifuatilia pambano hilo kwa ukaribu zaidi akiwa amevalia vazi la koti rasmi kabisa kwa ajili ya maafisa wa Manchester United akiwa karibu na benchi la ufundi la makocha karibu pia na wachezaji wa timu hiyo akiwemo Wilfied Zaha.

Hakuna uhakika ni namna gani David Moyes anajisikia kuwa nyuma ya mtu huyu mwasisi wa benchi la ufundi aliyestaafu kuwa nyuma yake wakati kikosi kikiwa katika nafasi ya nane katika msimamo wa ligi katika kipindi ambacho kimezoeleka United kuwa katika vita ya kupigania taji.

Looming: David Moyes is watched by a legend as Manchester United languish in eighth position in the table
David Moyes akifuatiliwa na meneja mstaafu.
Dressed to impress: Alex Ferguson watches on wearing a Manchester United coat and tie
Alex Ferguson akiwa katika vazi rasmi la maafisa wa United karibu na benchi la ufundi ndani akiwa na tai
All smiles: Alex Ferguson felt the festive cheer after seeing his old side come back from two goals down

Baada ya kuwa nyuma kimatokeo mapema kupitia kwa James Chester (mchezaji wa zamani wa United) na David Meyler, meneja huyo pengine angekuwa katika joto la mawazo nyuma yake kuna mtangulizi wake.
Hata United ilizinduka kwa kuandika goli la kichwa kupitia kwa Chris Smalling na lingine kupitia kwa Wayne Rooney na hivyo mpaka mapumziko timu hizo zilikuwa sare.
Chester akajikuta anatoka kuwa shujaa mpaka mkosefu 'hero to zero' kufuatia kujifunga goli katika kipindi cha pili na hivyo kuhitimisha hesabu ya mabao 3-2 United ikishinda kutoka nyuma kimatokeo.
Klabu hiyo yenye maskani yake Old Trafford sasa imejikita katika nafasi ya sita ikiwa nyuma kwa alama sita mbele ya vinara wa ligi hiyo Liverpool ambapo ushindi katika dimba la KC Stadium ulikuwa muhimu katika kurejesha matumani ya kuingia katika changamoto ya kutetea taji.
Hiyo imekuwa ndio nafasi ya chini kabisa kukaliwa na mashetani wekundu katika kipindi cha majira ya krismass katika historia ya ligi kuu Premier League.

One down: Hull take an unexpected early lead through former United player James Chester (centre)
Hull wakiandika bao la utangulizi kupitia kwa mchezaji wa zamani wa United James Chester (katikati)
Two down: David Meyler (centre) doubles Hull's first-half lead after seeing a shot deflected past David De Gea
David Meyler (katikati) akiandika bao la pili la Hull kipindi cha kwanza baada ya mpira kumgonga David De Gea
Comeback: Chris Smalling (3R) pulls one back for United with a towering header from a corner
Chris Smalling akifunga goli kwanza la United kwa kichwa baada ya mpira wa kona.here's looking at Roo: Wayne Rooney equalises with a screaming shot to send the teams in level at half-time
Wayne Rooney akiandika bao la kusawazisha la UnitedAgony and ecstasy: James Chester scores an own goal to the delight of Wayne Rooney
James Chester akijifunga na hivyo kuwapa United ushindi wa mabao 3-2 huku Wayne Rooney akishangilia

No comments:

Post a Comment