KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, December 6, 2010

Chris Hughton afukuzwa kazi na Newcastle United

Newcastle United imemfukuza kazi meneja wake Chris Hughton .
Tangazo la kufutwa kazi kwa meneja huyo limekuja baada ya Newcastle kupoteza mchezo wake mbele ya West Brom kwa kichapo cha mabao 3-1 matokeo ambayo yameiweka klabu hiyo katika nafasi ya 11 katika msimamo wa ligi kuu ya Uingereza “Premier League”.
Hughton ambaye ana umri wa miaka 51 aliingoza Newcastle mpaka kufikia nafasi ya juu msimu uliopita baada ya kuwa katika hali mbaya katika msimu wa 2008-09 .
Lakini wakati hali ikiwa hivyo klabu hiyo imekaririwa kupitia mtandao wa klabu wakisema kwasasa wanamsaka mtu ambaye atakuwa ana uzoefu na kazi za umeneja na kuweza kuwavusha katika nafasi nzuri huko mbele.
Taarifa imesema
"bodi ingependa kuweka rekodi na tunatoa shukurani kwa Chris kwa kipindi chote alichokuwepo klabu hapa tangu katika michuano ya Championship mpaka katika Premier League "

No comments:

Post a Comment