KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, April 1, 2012


Bayer yamfukuza kocha Dutt
Bayer Leverkusen imemfukuza kazi kocha wake Robin Dutt baada ya kichapo cha mabao 2-0 toka kwa Freiburg.
Klabu hiyo imetangaza hilo asubuhi ya leo na nafasi yake kushikiliwa na kocha Sami Hyypia, mlinzi wa zamani wa  Liverpool na bosi wa kikosi cha wachezaji vijana Sascha Lewandowski na watakalia nafasi hiyo kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo mpaka kumalizika kwa msimu.
Kichapo toka kwa Freiburg ni channe ikiwemo kichapo cha michuano ya ligi ya mabingwa toka kwa Bercelona cha mabao 7-1 on aggregate..
Wasaidizi wa Dutt Damir Buric na Marco Langner pia wameondoka klabuni hapo.
 
Bao la Robben laipa nguvu Bayern
Bao la Arjen Robben la dakika ya 69 lilitosha kuipa ushindi Beyern Munich dhidi ya Nurnberg katika mchezo ambao ulionekana kama kama Bavarian derby matokeo ambao yameisogeza Bayern Munich mbele zaidi kwa points tatu mbele ya Borussia Dortmund katika kilele cha ligi kuu ya nchini Ujerumani maarufu kama Bundesliga.
Mdutch huyo alifunga bao hilo katikati ya kipindi cha pili na kukipa kikosi cha kocha Jupp Heynckes ushindi waliokuwa wakiusaka na hivyo kuipa jakamoyo Dortmund wao wakiwa kileleni.
Hicho ni kipigo cha nne mfululizo kwa Nurnberg na kimewashusha kwa points tatu katika mstari wa hatari ya kushuka daraja na wakiwa wamesaliwa na michezo sita kabla ya kumalizika kwa msimu
Bayern inatarajia kukutna uso kwa uso na mabingwa mara sita wa taji la soka la nchini ujerumani Dortmund jumamosi ijayo.

Henry apiga hat-trick
Thierry Henry aliyerejea nchini marekani katika klabu yake ya New York Red Bulls ameendeleza makeke yake baaya ya kufunga mabao matatu ndani ya mchezo mmoja yaa “hat-trick” katika mchezo wa ushindi wa timu yake wa mabao 5-2 dhidi ya Montreal Impact katika ligi ya nchi hiyo MLS.
Nyota huyo wa zamani na mwenye heshima kubwa katika klabu ya washika bunduki wa Uingereza Arsenal alifunga bao lake la kwanza kunako dakika ya 28 akinyamazisha furaha ya wapinzani wao waliotangulia kwa bao la Sanna Nyassi lakini Justin Mapp akarejesha tena baadaye furaha ya Montreal kwa bao la pili la dakika ya 38 ya mchezo.
Kenny Cooper akafunga bao la penatina la kusawazisha  na kupelekea sare ya mabao 2-2 mpaka mapumziko  kabla ya Red Bulls kuanza karamu katika kipindi cha pili.


Henry alifunga bao lingine dakika ya 56 huku naye Mehdi Ballouchy akiongeza la nne kunako dakika ya 72 ikiwa ni dakika tatu tu baada ya kuingia akitoke benchi.
Henry alimalizia hat-trick dakika moja kabla ya mchezo kumalizika.
Katika mchezo mwingine Real Salt Lake ilipata mabao mawili katika dakika mbili za mwisho za mchezo na kuipa ushindi wa mabao 3-2 mbele ya Portland Timbers ushindi ambao umewaweka katika kilele cha msimamo wa ligi ya Western Conference.
Alvaro Saborio aliwapeleka wageni kwenye uongozi kunako dakika ya 38 kwa bao la mkwaju wa penati lakini  Darlington Nagbe aliweka mambo sawa baada ya mapumziko kwa Portland.
 

South Africa U-20 side beaten at home by Ghana

Timu ya taifa ya wanawake ya nchini Afrika kusini ya wachezaji wenye umri chini ya miaka U-20 maarufu kama Basetsana na si “banyana banyana” ambayo ni ya wakubwa  imekubali kichapo cha mabao 2-0 nyumbani toka kwa timu ya taifa ya Ghana ya wenye wenye umri huo ukiwa ni mchezo wa mzunguko wa pili wa michuano ya kusaka tiketi ya kufuzu fainali ya michuano hiyo dunia fifa 2012
Kichapo hicho cha wenyeji kimekuja wakiwa nyumbani katika mchezo uliopigwa Sinaba Stadium huko Daveyton.

Basetsana ilikuwa katika hali mbaya katika kipindi cha pili baada ya kupigwa mabao mawili toka kwa wafungaji Florence Dadson na Elizabeth Addo kiasi akina dada wa Ghana maarufu kama “Black Princesses” kuwa mbele kabla ya mchezo wa marudiano utakaopigwa wiki mbili zijazo.

Timu zote mbili katika cha kwanza zilikuwa katika kiwango safi na vinavyo fanana kabla ya Dadson katika kipindi cha pili kufunga bao la uongozi ikiwa ni dakika ya 50

Juhudi za Basetsana kusawazisha hazikuzaa matunda na zilzidi kupotea baada ya Patience Hlongwane kusababisha penalt akifanya madhambi katika eneo la hatari na yeye mwenyewe kutolewa nje kwa kadi nyekundu penati hiyo ilifungwa na Addo na kuwa bao la pili kwa ghana.

Kombe la dunia la FIFA la wachezaji wenye umri wa chini ya miaka U- 20 Women's World Cup 2012 litachezwa nchini Japan baadaye mwaka huu
 

No comments:

Post a Comment