KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, July 19, 2012

CAS imepindua kibano cha Mohamed Bin Hammam kufungiwa maisha kwenye soka

Bin Hammam
Nchi ya Qatari imepata ahueni ya kuendelea na kifungo cha maisha katika kujishughulisha na mambo ya mpira wa miguu kufuatia kushinda rufaa yake ya kupinga kufungiwa maisha kujishulisha na mchezo huo adhabu ambayo ilitolewaFIFA mwaka uliopita.
Mohamed Bin Hammam ambaye ni mwenyekiti wa soka nchini Qatar na aliyekuwa mjumbe wa kamati ya utendaji ya fifa alipata adhabu ya kutojihusisha na soka maisha lakini alikata rufaa katika mahakama ya usuluhishi ya michezo duniani (CAS) kupinga adhabu hiyo.
Qatari ilionekana kuwa na kosa kwa tuhuma za kutoa rushwa kwa maafisa wa soka wa Caribbean kwa lengo la kupambana na Sepp Blatter kuwania nafasi ya Rais wa FIFA na Bin Hammam akiwa ndiye mpinzani wake mkubwa.
Bin Hammam mara zote alikuwa akikanusha tuhuma hizo na sasa imethibitishwa na CAS, ambayo imesema wameshindwa kupata ushahidi wa kutosha juu ya tuhuma hizo dhidi yake.

No comments:

Post a Comment