Abdalah Kibadeni(King Kibadeni Mputa) |
Timu ya kagera sugar inayoshiriki ligi kuu ya
soka Tanzania Bara katika kuhakikisha inaboresha benchi lake la ufundi imeamua
kuongeza nguvu kwa kumchukua aliyekuwa kocha wa vijana wa Simba Abdalah
Kibadeni(King Kibadeni Mputa)
Akiongea na
Rockersports kocha msaidizi wa timu hiyo Mlage Kabange amesema timu yake inatarajia
kuingia kambini tarehe 20/07/2012 tayari kwa kujiandaa na ligi kuu ya Tanzania
Bara msimu wa 2012/2013 na kwamba Kibadeni atakuwa anachukua mikoba ya kocha wa zamani mganda Jackson Mayanja.
Kabange
amesema katika kuboresha kikosi chao msimu ujao Kagera Sugar pamoja na
kumchukua Kibadeni lakini pia imemsajili mlinzi wa kulia wa zamani wa mabingwa
wa soka Tanzania Bara Simba Salum Kanoni.
Kagera sugar pia imewasajili
wachezaji wawili wa kigeni toka nchini Nigeria, Benjamin Efee na Willfred Emee na
kumchukua mshambuliaji Daringtomi Enina toka Toto Afrika ya Mwanza.
Mlinzi wa zamani wa Simba Salum Kanoni |
No comments:
Post a Comment