KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, July 8, 2012

Giggs atajwa kuwa nahodha timu ya Olympic ya Great Britain

 
Kiungo wa Manchester United Ryan Giggs ametangazwa kuwa nahodha wa kikosi cha kocha Stuart Pearce kuongoza Great Brotain kwenye michezo ya Olympic.
Raia huyu wa Wales ni miongoni mwa wachezaji watatu wenye umri mkubwa zaidi ya miaka 23 ambao wanaruhusiwa kushiriki michezo hiyo akiungana wa waingereza wengine Craig Bellamy na Micah Richards kwenye Olympic London 2012.
Giggs ameshinda jumla ya mataji 12 ya Premier League,mataji manne ya FA na mataji mawili ya Champions Leagues ndani ya kipindi chake cha miaka 21 ya kucheza soka Old Trafford.
Giggs mwenye umri wa miaka 38 kwasasa amesema  "ni wazi nina uzoefu . kama nahodha nina matumaini ninaweza kuambukiza uzoefu wangu wachezaji vijana."
GB itacheza dhidi ya Brazil mchezo wa kirafiki July 20 katika uwanja wa 20 Middlesbrough wa Riverside Stadium.

Imepangwa katika kundi la A na nchi za Senegal, Uruguay na United Arab Emirates na itakuwa ikicheza michezo yake katika viwanja vya Old Trafford, Wembley na Millennium Stadium.


No comments:

Post a Comment