Kamati ya
sheria, hadhi na wachezaji ya shirikisho la soka nchini TFFimemruhusu mlinzi
wa zamani wa mabingwa wa soka Tanzania bara Simba Kelvin yondani kuendelea kuichezea
timu ya Yanga katika michuano ya Kombe la Kagame inayoendelea hivi sasa jijini
Dar es Salaam
Akizungumza
hii leo na waandishi wa habari mwenyekiti wa kamati hiyo Alex Mgongolwa amesema
maamuzi ya sekretarieti ya TFF kumruhusu
yondani kuichezea Yanga yliyofanywa na katibu wa TFF Angetile Oseah ni maamuzi sahihi kwa kuwa mkataba wa Simba na Yondani
umemalizika May 31 mwaka huu.
Mgongolwa
amesema Yondani tangu tarehe hiyo alikuwa huru na kwamba Simba waliwasilisha TFF
ombi la kumuongezea mkataba Yondani June 7 ambapo ni kinyume na taratibu za kuongezea
mkataba kwa mchezaji hivyo Yondani ruksa kuichezea Yanga.
Aidha katika
kuonyesha wapi mkanganyiko wa mkataba wa Yondani ulipoanzia Mgongolwa amesema mkataba
wapili wa Simba unaonyesha umesainiwa desemba 23 mwaka huu muda ambao haujafika
hivyo hauna athari kwa Yondani kutokuichezea Yanga kwenye michuano ya Kagame.
Hata hivyo
kamati hiyo imetoa rai kwa Simba na Yondani kukaa chini na wakubaliane kuhusu
mkataba huo wenye makosa.
Yondani |
haki imetendeka wazee wa kufoji mikataba poleni.waandaeni yoso wenu wazibe pengo badala ya kumng'ang'ania yondani
ReplyDelete