KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, July 25, 2012

MIKAKATI KUIMALIZA APR NUSU FAINALI SANGA ATETA NA VIONGOZI WA MATAWI JANGWANI.

Makamu mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga mwenye koti
Viongozi wa matawi  wa klabu ya Yanga wamekutana hii leo katika makao makuu ya klabu hiyo yaliyoko matika makutano ya mitaa Twiga na Jangwani Kariakoo jijini Dar es salaam kwa lengo la kujadili juu ya mipango ya kuimaliza APR ya Rwanda mchezo wa nusu fainali wa michuano ya kombe la Kagame kesho katika uwanja wa taifa.
Mkutano huo ulioitishwa na makamu mwenyekiti wa klabu hiyo Clement Sanga ulikuwa na ajenda kuu moja nayo ni kuhusu namna ya kumalizia michezo miwili ya kombe la Kagame na hatimaye klabu hiyo kufanikisha azma ya kutetea taji hilo.
Yanga imefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo baada ya juzi kuitoa kwa penati timu ngumu ya Mafunzo katika mchezo wa robo na sasa ikisubiri kukabiliana na mabingwa wa soka wa Rwanda APR mchezo ambao utatanguliwa na mchezo mwingine wa hatua hiyo ambao Azam fc itakuwa ikicheza dhidi ya timu alikwa ya Vita Club ya DRC.
Katika mkutano wa leo viongozi hao wa matawi wamekubaliana kimsingi kuunganisha nguvu zao katika kila hali ili kufanikisha lengo hilo.
Sanga amesema wao kama viongozi wapya wa Yanga bado hawajakaa kama kamati ya utendaji mbali na ukweli  kuwa ni wageni  katika kuingoza klabu hiyo kongwe hapa nchini, hivyo aliona ni vema kuwaita viongozi hao kujadiliana kwa pamoja namna ya kulinda taji hilo pale Jangwani.

Amewataka wapenzi na wanachama wa klabu hiyo kuiombea timu yao lakini pia wajitokeze kwa wingi kuishangilia na kuipa nguvu timu hiyo katika mchezo wa kesho ili waweze kuingia fainali na hatimaye kutwaa taji hilo.

No comments:

Post a Comment