KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, July 25, 2012

VIONGOZI WA MATAWI YANGA WAMTIMUA BHINDA MKUTANONII

Mohamed Bhinda akiwa na makamu mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga wakitete jambo.
Viongozi wa matawi ya klabu bingwa Afrika mashariki na kati ama mabingwa watetezi wa kombe la Kagame Yanga hii wamemgomea mjumbe wa kamati ya utendaji ya klabu hiyo Mohamed Bhinda kuketi katika meza kuu ya viongozi wa klabu hiyo wakati wa mkutano wa hii leo ulioitishwa na makamu mwenyekiti wa klabu hiyo Clement Sanga.
Mkutano huo ulioitishwa na Sanga ulikuwa na lengo la kupanga mikakati ya timu ya Yanga kutetea kombe la michuano ya Kagame kufuatia timu hiyo kufanikiwa kutinga katika hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo inayo endelea hivi sasa jijini Dar es Salaam na kesho wakikabiliwa na mchezo wa nusu fainali dhidi ya mabingwa wa soka wa Rwanda APR.
Katika mkutano huo wanachama wa Yanga waligoma katakata kumruhusu Bhinda kukaa meza kuu mzozo ambao ulichukua takribani saa nzima huku jitihada za makamu mwenyekiti Clement Sanga zikionekana kugonga mwamba.
Wanachama hao walikuwa wakitoa hoja kuwa Bhinda alikuwa ni msaliti katika kipindi cha uongozi wa aliyekuwa mwenyekiti wa klabu wakati huo Lyod Nchunga ambapo viongozi wenzake walikubali wakijiuzulu kwa shinikizo la wanachama wa klabu hiyo lakini yeye alitangaza kufanya hivyo mbele ya wanachama kisha baadaye akarejea kutokana na kutokuwepo na taarifa ya kujiuzulu kwake kimaandishi.
Sakata la leo lilikuwa kubwa lakini hatimaye busara ikatawala kikao hicho kwa jitihata za ziada za makamu  Sanga ndipo viongozi hao wa matawi  walipomruhusu kwa shingo upande kuketi katika meza hiyo.
Mbali na Bhinda mwingine aliyekutana na kadhia hiyo ni ni mwenyekiti wa matawi wa mkoa wa Dar es Salaam Mohamed Msumi ambaye alitakiwa kuondoka kabisa meza kuu kwa dhana ya muda wake wa uongozi kuwa umekwisha lakini akaokolewa na kura za viongozi hao wa matawi kujiridhisha kuwa muda wake bado unaendelea.
Viongozi hao wa matawi wamekubaliana kimsingi kuunganisha nguvu zao katika michezo ya nusu fainali na fainali ya kombe la Kagame endapo timu hiyo itafanikiwa kuifunga APR katika mchezo wa kesho uwanja wa taifa huku mchezo mwingine wa hatua hiyo mchana saa nane utakuwa ni baina ya Azam na Vita Club ya DRC.

No comments:

Post a Comment