Liverpool imeanza
vibaya mchezo wa kwanza wa kujiandaa na msimu mpya wa ligi baada ya kuchapwa
kwa bao 2-1 na Roma ya Italia mbele ya mashabiki waliojazana katika uwanja wa Fenway
Park.
mashambulizi
mawili ya kipindi cha pili kupitia kwa Michael Bradley na Alessandro Florenzi
yalidhihirisha kuwa Giallorossi wako sawa licha ya jitihada za dakika za mwisho za Liverpool
kupitia kwa kiungo Charlie Adam.
Bosi wa Liverpool
Brendan Rodgers aliamua kuwatumia katika kikosi cha kuanzia Raheem Sterling na Nathan
Eccleston sehem ya ushambulizi wakati wazoefu Martin Skrtel, Jamie Carragher na
Joe Cole wakiwa sehemu ya kiungo. Wakongwe Francesco Totti na mshambiliaji Pablo
Osvaldo walianza kwa upande wa Roma huku Zdenek Zeman akionekana kuwa imara
katika kikosi hicho.
No comments:
Post a Comment