Chelsea
imekamilisha usajili wa kiungo mshambuliaji Oscar na kuingia nae mkataba wa miaka mitano kwa ada
ya uhamisho ya pauni milioni £25m.
Mbrazil huyo
ambaye kwasasa yuko nchini Uingereza kwenye michuano ya Olympic akiwa na kikosi
cha Brazil anajiunga na Chelsea akitokea Internacional na huko nyuma alikuwa
akiitumikia Sao Paulo.
Kiungo huyo mwenye
umri wa miaka 20 amekuwa akifananishwa na mbrazil mwenzake Ricaldo Kakal.
Mabingwa hao
wa vilabu ulaya Chelsea tayari wameshakamilisha usajili wa Marko Marin na ndugu
wawili Eden na Thorgan Hazard majira haya ya uhamisho wa kiangazi.
Oscar huko
nyuma aliarifiwa kusubiri mpaka kumalizika kwa Olympics kabla ya kuakmisha
taratibu za usajili kujiunga na kikosi cha Roberto Di Matteo lakini inaonekana
mambo yameharakishwa tofauti na ilivyokuwa imepangwa.
No comments:
Post a Comment