Mwanariadha
aliyetumainiwa kushinda medali ya dhahabu kwa kasi yake na uhodari katika mbio
za mita 1500 Mariem Alaoui Selsouli hatoshiriki mashindano ya Olimpiki kwa
kupatikana kua alitumia dawa ya kuongezea nguvu mwilini.
Selsouli
mwenye umri wa miaka 28 alishinda medali ya fedha kwenye mashindano ya Dunia
mwaka huu alipatikana kutumia dawa iliyopigwa marufuku aina ya furosemid
kupitia vipimo vilivyochukuliwa tareh 6 Julai mjini Paris.
Mariam Alaoui
amewahi kufungiwa kwa kutumia dawa za kuongezea nguvu mwilini na safari hii
huenda akafungiwa maisha.
Katika
taarifa yake, Shirikisho la michezo ya Riadha duniani IAAF limetangaza kuwa
aina ya dawa ya furosemide iligundulika mwilini mwa mkimbiaji huyo.
Kulingana na
Sheria za IAAF bado mwa\nariadha huyo ana haki ya kuomba kesi isikilizwe ambapo
chama cha riadha cha Morocco kinatakiwa kuhudhuria.
No comments:
Post a Comment