Shirikisho
la soka nchini Tff limeingia mkataba wa miaka mitatu na BancABC kwa ajili ya kuandaa
mashindano yenye lengo la kuziandaa timu mbalimbali kwa ajili ya msimu mpya wa
ligi kuu za Tanzania Bara na Zanzibar (yaani pre season) ambayo yatakuwa yakiitwa
BancABC
sup8r Soccer tournament 2012.
Wakiongea
hii leo mbele ya waandishi wa habari katibu wa TFF Angetile Oseah na mkuu wa kitengo
cha fedha wa banki ya ABC Mwalimu Zuberi aliyeambatana na mkurugenzi wa benki
hiyo Bornface Nyoni wamesema lengo kuu la mashindano hayo ni kutoa zawadi kwa wateja
wa benki yao mbali ya kutoa burudani lakini pia ni kutimiza tamko la serikali kwa
wawekezaji makampuni na taasisi binasfi kujihusisha na michezo.
Mashindano
hayo ambayo kwa mwaka huu yamepangwa kufanyika kuanzia August 4 mpaka 18 yatakuwa
yakifanyika katika vituo vinne vya Dar es Salaam , Arusha ,Mwanza na Zanzibar na
yatakuwa yakishirikisha jumla ya timu nane ambazo ni zile zilizo shika nafasi tatu
za juu katika ligi kuu ya Vodacom(Tanzania Bara) na nyingine tatu za juu katika
ligi ya Zanzibar.
Timu
nyingine ni mbili ni zile zilizo panda daraja toka kila upande moja kutoa
Tanzania Bara na nyingine kutoka Zanzibar.
Mkataba wa
TFF na Benki hiyo ni wa miaka 3 lakini hata hivyo haijawekwa wazi unathamani ya
kiasi gani kutokana na kile kilichoelezwa kuwa kutakuwa na mabadiliko kila
mwaka.
Katibu wa
TFF Angetile Oseah amesema tayari amesha viandikia barua vilabu vyote kuwajulisha
juu ya hilo licha ya kushindwa kuthibitisha juu ya kama wamekubalia ama la.
No comments:
Post a Comment