KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, July 19, 2012

Pre-season: AmaZulu 0-1 Manchester United

Federico Macheda
Federico Macheda alifunga bao pekee la Manchester United dhidi ya AmaZulu wakati timu hiyo ikianza ziara ya matayarisho ya msimu mpya wa ligi 2012/2013 nchini Afrika Kusini.
mshambuliaji huyo Mtaliano alifunga goli hilo akiwa pembeni mwa uwanja kunako dakika ya 19.
lakini katika mchezo huo United ilikuwa ikishambiliwa sana kiasi mlinda mlango Anders Lindegaard akilazimika kuokoa michomo kadhaa ikiwemo mpira wa kichwa wa Josef Letka.

Shinji Kagawa kiungo mpya wa timu hiyo aliingizwa zikiwa zimebakia dakika mbili mpira kwisha.

Bosi wa United Sir Alex aliwatumia wazoefu katika timu yake kama vile Rio Ferdinand, Paul Scholes, Michael Carrick, Javier Hernandez na Dimitar Berbatov anajaribu kutafuta kiwa cha kiushindani zadi katika kipindi hiki cha maandalizi ya kuanza ligi ya Uingereza.

No comments:

Post a Comment