KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, October 12, 2012

HATMA YA UCHAGUZI WA CHAMA CHA SOKA MKOA WA DAR ES SALAAM KUJULIKANA JUMANNE.

UCHAGUZI WA CHAMA CHA MPIRA WA MIGUU MKOA WA DAR ES SALAAM (DRFA)
Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imekamilisha usikilizaji rufani zilizokatwa dhidi ya Kamati ya Uchaguzi ya DRFA.
 
Ili kujiridhisha kuhusu uamuzi wote uliofanywa na Kamati ya Uchaguzi ya DRFA kuhusu waombaji uongozi wote wa DRFA waliopitishwa na ambao hawakupitishwa na Kamati ya Uchaguzi ya DRFA, Kamati itatangaza uamuzi wake kuhusu mchakato mzima wa uchaguzi wa DRFA siku ya Jumanne, Oktoba 16, 2012.
 
Kutokana na hali hiyo, Uchaguzi wa DRFA uliokuwa ufanyike Oktoba 14, 2012 umeahirishwa hadi hapo uamuzi kuhusu uchaguzi huo utakapotangazwa Jumanne, Oktoba 16, 2012.
 
Angetile Osiah
Katibu Mkuu
Katibu- Kamati ya Uchaguzi TFF

No comments:

Post a Comment