KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Wednesday, October 10, 2012

VERMAELEN ANA AMINI WILSHERE NI MIONGONI MWA VIUNGO BORA DUNIANI.


Thomas Vermaelen anaamini kuwa Jack Wilshere ana uwezo wa kuwa mmoja kati ya viungo hodari dunaini.

Kiungo huyo alikuwa nje ya uwanja kwa takribani miezi 14 akisumbuliwa na maumivu ya enka na mguu lakini amerejea akiwa vizuri katika kikosi cha timu ya taifa ya wachezaji wenye umri chini ya miaka 21.

Amenukuliwa na mtandao wa klabu hiyo akisema Vermaelen akisema,
"unajua alichokifanya katika msimu wake mzima wa kwanza akiwa na Arsenal, alifanya vitu vikubwa sana”. 

"kwa upande wangu anaweza kuwa mmoja kati ya viungo bora kabisa duniani. Ana uwezo mkubwa wa kufikia hapo.

"ninafuraha sana amerejea sasa. Anafanya kazi ya kurejesha uwezo wake kama zamani na hilo ni jambo muhimu. Nadhani baadaye ataibeba timu hii."

No comments:

Post a Comment