KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, November 16, 2012

KIMATAIFA:ROONEY ANA NDOTO YA KUVUNJA REKODI YA SIR CHARLTON YA KUPASIA NYAVU, JOHN TERRY MKOSI JUU YA MKOSI, DANTE UMRI UMEKWENDA HAJAWAHI KUSHINDA TAJI SASA ANASEMA AMECHOKA KUUZA SURA NA BECHKAM KWELI ATAKWENDA AUSTRALIA NA KUONDOKA GALAX? SOMA ZOTE HAPA.

NITAIVUNJA RIKODI YA SIR CHARLTON YA KUPASIA NYAVU MAN UNITED NA TIMU YA TAIFA


Wayne Rooney amedhamiria kuivunja rekodi ya ufungaji iliyowekwa na Sir Bobby Charlton katika klabu ya Manchester United na timu ya taifa ya England.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 kwasasa yuko katika nafasi ya nne ya wafungaji bora waliowahi kupita United akiwa ameshafumania nyavu mara 185 ambayo ni pungufu ya mabao 64 ya Charlton ambaye anaendelea kushikilia rekodi ya ufungaji ya klabu hiyo ya mabao 249.

Katika timu ya taifa ya England ‘Three Lions Rooney’ Rooney amefunga jumla ya magoli 32 ambayo ni pungufu mabao 17 kufikia rekodi ya Charlton ya mabao 49.

Amekaririwa Rooney akisema
"Sir Bobby anashikilia rekodi zote mbili,  hii ni changamoto kubwa sana, jamaa ni mwasisi katika klabu kwahiyo ni kama mtu ambaye anaendelea kuwepo katika klabu, kama nitafanikiwa kuvunja rekodi yake ya ufungaji bora katika klabu na hata katika timu ya taifa hilo litakuwa ji jambo la kupendeza."

Rooney pia anataka kucheza soka katika kipindi kirefu zaidi kama ilivyo kwa Ryan Giggs na Paul Scholes wachezaji ambao wanamvutia kwa kuendelea kuwepo kwa zaidi ya muongo mmoja.

Nahodha wa Chelsea Terry nje kwa wiki tatu 
Meneja wa Chelsea Roberto Di Matteo amethibitisha kuwa John Terry atakuwa nje ya uwanja kwa takribani wiki tatu kufuatia kuwa majeruhi wa mguu.

Kuna wasiwasi kuwa huenda mlinzi huyo wa kati akaendelea kuwa nje kwa kipindi kirefu zaidi kutokana na kuwepo taarifa kuwa mguu wake ambao aligongana na mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez katika mchezo wa jumapili uliomalizika kwa sare ya bao 1-1, kupinda kidogo.

Mlinzi huyo wa kimataifa wa England alionekana akigumia kwa nguvu kutokana na maumivu na kisha kutolewa nje kwa kutumia machela katika dimba la Stamford Bridge ambapo kipimo cha 'MRI scans' hapo kabla kikonyesha alipatwa na madhara kidogo katika mshipa wa mguu.

Hata hivyo bosi wa ‘The Blues' Di Mateo ametanabaisha kuwa mlinzi huyo mwenye umri wa miaka 31 atakosekana kwa wiki tatu jambo ambapo amesema ni pigo kwa kikosi chake.

Dante: Nimekuja Bayern kusaka mataji na si kuuza sura
Mlinzi wa kati wa Bayern Munich Dante amesema waziwazi kuwa kilichomshawishi kujiunga na klabu hiyo si kingine isipokuwa anahitaji kushinda mataji.

Mlinzi huyo wa zamani wa Borussia Monchengladbach alijiunga na Bavaria kwa ada ya euro million 4.7 katika kipindi cha uhamisho wa kiangazi baada ya kuipa mafanikio Gladbach katika msimu wa 2011-12 ambapo ilimaliza katika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi ngumu kabisa ya nchini Ujerumani ‘Bundesliga’.

Akiwa hajawahi kushinda taji lolote kubwa katika soka , mlinzi huyo mwenye umri wa miaka 29 anafikiria ndoto yake itatimia kwa kujiunga na kikosi cha kocha Jupp Heynckes.
 
Beckham hana mpango wa kuondoka LA Galaxy na kuelekea Australia
Msemaji wa Kiungo na nahodha wa zamani wa England David Beckham amekanusha taarifa kuwa mchezaji huyo ana mpango wa kuihama klabu yake ya LA Galaxy na kuelekea nchini Australia baada ya shirikisho la soka nchini Australia (FFA) kudai kuwa kiungo huyo ambaye kwasasa ana umri wa miaka 37 alikuwa anaitamani ligi kuu ya soka ya nchi hiyo ya A-League.

Msemaji wa FFA amedokeza kuwa mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United alikuwa katika mpango wa kufuata nyayo za akina Alessandro Del Piero na Emile Heskey na kujiunga na soka la Australia.

Taarifa kupitia msemaji wa FFA ambazo zilionyesha ni kama kuifagilia ligi ya Australia imesomeka
"kuja kwa David Beckham ni ishara kuwa hadhi ya ligi yetu ya Hyundai A-League imekuwa duniani.

"Beckham ni nyota mkubwa sana duniani na atakuwa mtu mwingine mkubwa katika soka kujiunga na Hyundai A-League baada ya kuja kwa Alessandro Del Piero, Emile Heskey na Shinji Ono. Lakini kwasasa ujio wake bado uko katika hatua za awali"

Hata hivyo msemaji wa Beckham amekanusha taarifa hizo akisema mchezaji huyo kwasasa ana furahia maisha katika jiji la Los Angeles na hana mpango wa kuondoka.

No comments:

Post a Comment