KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, November 23, 2012

XABI ALONSO: CRISTIANO RONALDO SIO DIVA SINA URAFIKI NAYE NJE YA UWANJA. RONALDINHO KUENDELEA NA MINEIRO NA JOE COLE NIMEPONA SASA MTANIKOMA.

Kiungo wa Real Madrid Xabi Alonso amesema hana urafiki wowote na Cristiano Ronaldo lakini ni watu ambao wanaheshimiana.

Tangu kuanza kwa msimua kulikuwepo na tetesi zinazo husiana na mahusinao ndani ya kambi ya Madrid ambapo baadaye Ronaldo akaibuka mbele ya umma na kuweka wazi juu ya anavyokosa raha ndani ya klabu hiyo.

Kiungo huyo wa zamani wa Liverpool ndiye mchezaji wa hivi karibuni kunukuliwa akiweka wazi hali ya ukaribu wake na mshambuliaji huyo wa zamani wa Manchester United na kusema wazi kuwa urafiki wake na Ronaldo haundelei nje ya uwanja.
“baina yangu mimi na yeye ni watu ambao tuna heshimiana na kila mmoja kumkubali mwenzake ”
“wazi kabisa si kila mtu ni rafiki yangu nje kambi na pengine huko nje ni kwamba kila mtu ana mambo yake hakuna ukaribu kabisa lakini ndani ya chumba cha kubadilishia nguo tuko pamoja. Cristiano sio diva."

Katika hatua nyingine, Alonzo amesisitiza umuhimu wa nahodha huyo wa timu ya taifa ya Ureno katika kikosi cha Real Madrid na hakuna kingine isipokuwa maneno mazuri kwa kocha Jose Mourinho.

"ni mchezaji mwenye nia na mwenye kujiamini. Ni mchezaji muhimu katika timu"
"kila siku najifunza kutoka kwa Mourinho. Ni mtu mwenye kutaka na anazingatia kila kitu.

“watu wanadhani wanamjua lakini naona wanamuangalia kwa muonekano wa nje. Namfahamu ndani ya chumba cha kubadilishia nguo ni mtu tofauti sana.”

Ronaldinho kuingia mkataba mpya na Atletico Mineiro.
Kiungo mbrazili Ronaldinho Gaucho anajipanga kufanya mazungumzo ya kuingea upya mkataba na klabu yake ya Atletico Mineiro wiki ijayo.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 32 alikuwa akihusishwa na kutaka kuelekea katika vilabu vya Fluminense na Santos baada ya kuonyesha kiwango safi jambo ambalo limepelekea klabu yake kumtayarishia mkataba mwingine haraka haraka.

Wakala wa Ronaldinho ambaye pia ni kaka yake Roberto Assis amerudia kauli yake kuwa atatoa taarifa rasmi  lakini kwasasa mpango huo uko katika hatua za mwishoni.

Ronaldinho bado ana matumaini ya kurejea katika kikosi cha timu ya taifa ya Brazil, na kulikuwepo na tetesi kuwa uhakika wa kupata nafasi katika klabu yake ya Atletico Mineiro ndiyo sababu kubwa inayo mfanya asiondoke katika klabu hiyo.

Joe Cole: Bado nitaendelea kuwepo Liverpool.
Joe Cole anaamini kuwa bado ana nafasi ya kuendelea kuwepo Liverpool baada ya kuonyesha soka safi katika mchezo dhidi ya Young Boys mchezo wa michuano ya ligi ya Ulaya.

Cole alifunga goli moja na kusababisha lingine katika mchezo ambao ulimalizika kwa sare ya mabao 2-2 mchezo uliofanyika Anfield.

Cole mwenye umri wa miaka 31 anasema alikuwa katika kiwango safi katika vilabu vingine kabla ya Liverpool na amesisitiza kuwa anarejesha uwezo wake baada ya kufanikiwa kurejesha uimara wa mwili wake kimazoezi na kuponya majeraha ya msuli.

“nilikuwa mchezaji mzuri West Ham, Chelsea na Lille nadhani nitakuwa mchezaji mzuri Liverpool pia,”
"ninaimarika katika kila mchezo.
 Ni kawaida mchezaji kutaka kucheza kila mchezo. Huu ulikuwa mchezo wangu wa tatu kutoka katika maumivu ya msuli najisikia vizuri."

No comments:

Post a Comment