KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, November 8, 2012

Xavi: tusahau kipigo cha Celtic tuiangalie Spartak ,Wilshere, Sterling, Shelvey & Osman watajwa kikosi cha England , Ibrahimovic amesimamishwa michezo miwili ya Ligue 1 na Sergio Ramos anasema anacheza mpira akiwa katika maumuvu makali kwa kuwa wachezaji wengi ni majeruhi.



Xavi Henandez amesema klabu yake ya Barcelona ya kichapo cha mabao 2-1toka kwa Celtic na sasa kuangalia mchezo wao ujao dhidi ya Spartak Moscow bila kujali matokeo yakushangaza yaliyopita.


Barcelona ilikamuliwa na mabingwa hao wa uskochi Celtic katika dimba la Celtic Park wa jana jumatano ambapo kiungo huyo wa kimataifa wa Hispania anaamini kuwa wanapaswa sasa kuondoa vichwani mwao kichapo hicho na kuangalia mbele safari yao ya Urusi kuwafuata Spartak Moscow Novemba 20.

“mchezo muhimu sasa ni kule Moscow, tunapaswa kuwa katika uongozi wa kundi ”
“tumekosa nafasi hiyo dhidi ya Celtic, sasa itategemea na sisi wenyewe. Tunapaswa kuelekea huko kusaka ushindi ukiwa ni mmoja wa michezo yetu miwili iliyosalia”

Baada ya mchezo dhidi ya Spartak, kikosi cha kocha Tito Vilanova kitarudi nyumbani kucheza dhidi ya Benfica Camp Nou hiyo itakuwa Desemba 5.

Licha ya kufunga hiyo jana bado Barcelona imeendelea kukalia usukani wa kundi G wakiwa na alama tisa alama mbili zaidi ya Celtic, alama tano zaidi ya Benfica na alama sita zaidi ya Spartak.

Sergio Ramos anasema anacheza mpira akiwa katika maumuvu makali kwa kuwa wachezaji wengi ni majeruhi.
Mlinzi wa Real Madrid Sergio Ramos amesema amekuwa akikabiwa na maumivu lakini amekuwa akicheza kwa kuzuia maumivu kusaidia kikosi cha timu yake ambayo imekosa mlinzi aliye ambaye yuko fiti.

Wenzake walinzi wa pembeni Marcelo na Fabio Coentrao bado wanaendelea kusumbuliwa na majeraha wakati huu ambapo Alvaro Arbeloa pekee ndiye aliyerejea baada ya kuwa nje ya uwanja kwa muda sasa.

Ramos amesisitiza kuwa ameamua kucheza licha ya kuwa na maumivu ya misuli kwakuwa asingependa kuwaangusha wenzake.

"ni kweli siko katika hali nzuri kwa asilimia 100 na hii ni kutokana na maumivu ya misuli, huu si wakati wa kuacha kucheza kwasababu tuna wachezaji wengi muhimu majeruhi katika eneo la ulinzi. Tunapaswa kuwepo pale kama timu"

Ramos mwenye umrik wa miaka 26 ametoa huduma mara 15 katika kikosi cha Madrid tangu kuanza kwa msimu huu.

Ibrahimovic amesimamishwa michezo miwili ya Ligue 1 
Zlatan Ibrahimovic amesimamishwa kucheza michezo miwili kufuatia kutolewa nje ya uwanja katika mchezo baina ya Paris Saint-Germain dhidi ya Saint Etienne mchezo ambao walifungwa mabao 2-1 jumamosi iliyopita.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31 alionyeshwa kadi nyekundu ya moja kwa moja iliyotokana na kumchezea vibaya mlinda mlango Stephane Ruffier baada ya kunyanyua daruga kifuani kwake katika harakati za kuwania mpira.

Mwenyekiti wa LFP Pascal Garibian amesema adhabu hiyo imechukuliwa kama mgongano baina ya wachezaji hao ulikuwa kama ajili.

"Ibrahimovic amesimama kwa michezo miwili kwa kucheza rafu mbaya ambayo imehatarisha hali ya mchezaji mwenzake "

Ibrahimovic atakosekana katika mchezo dhidi ya mabingwa wa taji la ‘League 1’ Montpellier jumamosi hii pamoja na mchezo dhidi ya Rennes Nov. 17. 

Ibrahimovic amefunga jumla ya mabao 10 katika Ligue 1 msimu huu na kukisaidia kikosi cha kocha Carlo Ancelotti kukalia usukuani wa ligi ya nchini Ufaransa wakiwa na alama 22 baada ya michezo 11.

 Wilshere, Sterling, Shelvey & Osman watajwa kikosi cha  England
Kiungo wa Arsenal Jack Wilshere ameitwa tena kuunda kikosi cha timu ya taifa ya soka ya England tayari kwa mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Sweden.

Wilshere mwenye umri wa miaka 20 amerejeshwa kikosini baada ya kuwa majeruhi kwa zaidi ya mwaka mmoja ambapo aliitumikia England mchezo mmoja.

Wapo wachezaji ambao wameitwa kwa mara ya kwanza ikiwa ni pamoja na kiungo wa Everton Leon Osman, Raheem Sterling wa Liverpool na kinda Jonjo Shelvey.

Nahodha wa Liverpool Steven Gerrard yupo kikosini kwa mara nyingine tena na anatarajiwa kuwa mchezaji wa sita wa England kutimiza michezo 100 ya kuitumikia timu ya taifa.

Wachezaji wengine ambao huko nyuma waliwahi kuichezea timu ya taifa kwa zaidi ya michezo 100 ni pamoja na Peter Shilton aliyechezea michezo 125,David Beckham michezo 115, Bobby Moore michezo 108, Bobby Charlton michezo 106 na Billy Wright jumla ya michezo 105.

Kikosi cha sasa kinabadiliko ya wachezaji 10 tofauti na kile kilichocheza mchezo wa kuwania kufuzu kombe la dunia dhidi ya Ukraine na Poland.

Ashley Cole ambaye ameshaitumikia England jumla ya michezo 99 ameachwa kutokana na kutokuwepo katika kikosi cha Chelsea kulichokuwepo dimbani katika mchezo dhidi ya Shakhtar Donetsk hapo jana akisumbuliwa na maumivu ya msuli.

Joleon Lescott, Adam Johnson, James Milner, Andy Carroll, Kieran Gibbs, Michael Carrick, Frank Lampard, Alex Oxlade-Chamberlain na Jermain Defoe wote hawatakuwepo katika mchezo huo utakaopigwa mjini Stockholm.

Goalkeepers: Fraser Forster (Celtic), Joe Hart (Manchester City), John Ruddy (Norwich City).
Defenders: Leighton Baines (Everton), Ryan Bertrand (Chelsea), Gary Cahill (Chelsea), Steven Caulker (Tottenham), Phil Jagielka (Everton), Glen Johnson (Liverpool), Ryan Shawcross (Stoke City), Kyle Walker (Tottenham).
Midfielders: Tom Cleverley (Manchester United), Steven Gerrard (Liverpool), Aaron Lennon (Tottenham), Leon Osman (Everton), Jonjo Shelvey (Liverpool), Raheem Sterling (Liverpool), Theo Walcott (Arsenal), Jack Wilshere (Arsenal), Ashley Young (Manchester United).
 Forwards: Wayne Rooney (Manchester United), Daniel Sturridge (Chelsea), Daniel Welbeck (Manchester United).

No comments:

Post a Comment