KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, December 29, 2012

SIMBA YAKONG'OTWA NA TUSKER YA KENYA TATU BILA

Beki wa Tusker Mark Odhiambo (kushoto), akimiliki mpira wa juu kwa kichwa mbele ya mshambuliaji wa Simba Abdallah Juma wakati wa mechi ya kirafiki kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.Tusker imeshinda mabao 3-0.
Mabingwa wa soka Tanzania Bara wekundu wa Msimbazi Simba hii leo wamekubali kichapo cha mabao 3-0 toka kwa mabingwa wenzao wa nchini Kenya Tusker katika mchezo uliofanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Simba ambayo iliwatumia zaidi wachezaji wake wa kikosi cha pili hususani katika kipindi cha kwanza ikiwa chini ya makocha makocha Moses Basena na Jamhuri Kihwelu ilikubali mabao mawili katika kipindi hicho yaliyofungwa na Jesse Were kunako dakika za 37 na 45.
Tusker iliandika bao la tatu kunako dakika ya 54 lilofungwa na Frederick Onyango.
Simba ambayo inajiandaa na safari ya kuelekea Zanzibar kushiriki michuano ya kombe la Mapinduzi ilikuwa ikicheza mchezo huo bila ya mpangilio wa kueleweka ikiwatumia akina Haruna Shamte, Haruna Athumani, Paul Ngalema, Mussa Mudde, Abdallah Seseme, Abdallah Juma, Ramadhani Chombo, Kiggi Makassy na Miraj Adam.
Wengine ni Hassan Isihaka, Emily Ngeta, Jonas Mkude, Salim Kinje, Haruna Moshi, Ramadhani Singano, Nassor Masoud ‘Chollo’ na Edward Christopher.

Simba hii leo iliwakosa wachezaji wake muhimu kadhaa kama Juma Kaseja, Shomari Kapombe na Emmanue Okwi.

Tusker FC iliwatumia Samuel Odhiambo, Luke Ochieng, Jeremiah Bright, Mark Odhiambo, Joseph Shikokoti, Khalid Aucho, Edwin Manono, Frederick Onyango, Ismail Dunga, Jesse Were, Robert Omonuk, 
Baada ya mechi hiyo Kocha wa Tusker Robert Matano alisema kwamba hatua ya timu yake kupata ushindi katika mechi mbili ngumu, imempa faraja ya kunyakua ubingwa wa Kombe la Mapinduzi inayotarajia kuanza January 01 mwaka 2013 visiwani Zanzibar.
Naye Kocha wa Simba Julio alisema kwamba hatua ya Simba kupotea mechi hiyo imempa nafasi ya kujua makosa ya timu na atayarekebisha kabla ya kombe la Mapinduzi kuanza.

No comments:

Post a Comment