KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, December 27, 2012

UKURASA WA HABARI ZA KIMATAIFA:Bale afurahia Hat trick yake ya kwanza ‘Premier League’,Newcastle huenda ikakumbana na rungu la FIFA.Blackburn yamfuta kazi meneja wake Henning Berg baada ya kutumikia siku 57 kama bosi na Rodgers: hatukustahili lolote dhidi ya stoke city.



Winga wa Tottenham Gareth Bale amefurahia kufanikiwa kufunga mabao matatu ya kwanza katika mchezo mmoja ‘Hat trick’ katika ligi kuu ya soka ya England ‘Premier League’ lakini anasema kikubwa ulikuwa ni ushindi ambao uliipatia alama tatu muhimu Spurs baada ya kuichapa Aston Villa mabao 4-0 hapo jana.


Jermain Defoe alifunga goli la kwanza kwa Spurs kunako dakika ya 58 kabla ya Bale kufunga magoli mengine matatu yaliyowapa uhakika wa ushindi katika mchezo huo.


Vijana hao wanaotoka London ya Kaskazini waliingia katika mchezo huo wakiwa na kumbukumbu ya sare ya bila kufungana dhidi ya Stoke, ambapo walikuwa wakijua wazi kwamba muhimu kwao ulikuwa ni ushindi ili kuendelea kuleta ushindani katika nafasi ya juu katika msimamo wa ligi.


Akinukuliwa kupitia ukurasa wa mtandao wa kijamii wa twitter  wa klabu yake, Bale amesema,

 "vizuri kufunga magoli na kupata ‘hat trick’ yangu ya kwanza katika ‘Premier League’ lakini muhimu ni kupata alama 3".

"wachezaji wote walifanya kazi nzuri, sasa tunajipanga kwa ajili ya mchezo na Sunderland"

Kwa upande wake meneja Andre Villas-Boas amepongeza vijana wake walivyokuwa uwanjani tangu kuanza kwa mchezo mpaka mwisho



Newcastle huenda ikakumbana na rungu la FIFA.
  Newcastle na Millwall huenda wakakumbana na adhabu ya shirikisho la soka duniani FIFA kufuatia vilabu hivyo kugomea kuwaachia wachezaji wa kimataifa wa Nigeria  Shola Ameobi na Danny Shittu kwa ajili ya kulitumikia taifa lao katika michuano ya fainali za mataifa ya Afrika nchini Afrika Kusini mwezi Januari

Bosi wa Newcastle Alan Pardew anasema mshambuliaji wake Shola Ameobi hatasafiri kuelekea Afrika katika fainali hizo.


Ameobi na Shittu wote wanatarajiwa kujitoa rasmi katika uteuzi wao katika timu ya taifa ya Nigeria (Super Eagles), jambo ambalo limeonekana kulikasirisha shirikisho la soka la nchi hiyo (NFF).


Meneja wa Newcastle Alan Pardew amesema Ameobi hatatokezea katika michuano hiyo ambayo inatarajiwa kuanza January 19, wakati ambapo mlinzi wa Millwall er Shittu naye anatarajiwa kutolea nje uteuzi wake kama ilivyo kwa Ameobi.


Sheria za FIFA zinasema mchezaji yoyote ambaye atashindwa kuripoti katika timu yake ya taifa baada ya kutajwa na nchi yake kwa ajili ya majukumu ya kimataifa , basi mchezaji huyo atakuwa si halali kutumika katika kipindi chote kilichopendekezwa wakati wa jukumu hilo pamoja na kuongezewa siku tano zaidi kama itawezekana vinginevyo kuwepo na makubaliano mengine kati ya klabu yake na nchi husika.


Mjumbe wa bodi ya shirikisho la soka la Nigeria Chris Green amesema watahakikisha klabu za wachezaji hao zinaadhibiwa kama watagomea kuwaachia wachezaji hao.



 Blackburn yamfuta kazi meneja wake Henning Berg baada ya kutumikia siku  57 kama bosi.
 Blackburn Rovers imemfukuza kazi meneja wake Henning Berg na maafisa wengine watatu katika safu ya makocha ikiwa ni hatua ambayo imefuatia klabu hiyo kutereza katika vibaya katika msimamo wa ligi ndogo ya nchini England, Championship.


Meneja huyo raia wa Norway, ambaye aliajiriwa mwezi  October, katika jumla ya michezo 10 amefanikiwa kushinda mchezo mmoja tu katika kipindi chake cha utumishi wake wa siku 57.


Berg, ambaye alikuwa mchezaji wa Rovers mwaka 1995 wakati huo Rovers ilishinda taji la ligi kuu ya England “Premier League”  na baadaye akishinda taji la “League Cup” akiwa nahodha wa kikosi mwaka 2002, alirejeshwa katika klabu hiyo kama meneja mwezi Oktoba.

Baada ya Blackburn kuanza kwa kusuasua chini ya meneja wake wa zamani Lyn Oslo na Lillestrom klabu hiyo ikaamua kumpa Berg jukumu la kukinoa kikosi hicho katika kipindi hiki cha mwisho wa mwaka.

Kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Middlesbrough jana Boxing Day kilipelekea Rovers kujikuta katika nafasi ya 17 ikifanikiwa kukusanya alama 7 ndani ya uwezo wake wa kukusanya alama 30 kama wangeshinda michezo yote chini ya meneja Henning Berg.


Meneja msaidizi, Eric Black, kocha wa namba moja Iain Brunskill kocha wa makipa Bobby Mimms nap wamekumbwa na dhahma hiyo ya kufukuzwa kazi pamoja na Berg kutoka katika viunga vya Ewood Park.



Rodgers: hatukustahili lolote dhidi ya stoke city.
 Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers amesisitiza kuwa hawakuwa na la kujivunia katika mchezo ambao walipoteza kwa kuchapwa mabao 3-1 na Stoke City iliyocheza vema hapo jana kule katika dimba la Britannia jioni ya jana.


Wekundu hao walipata bao la mapema kupitia kwa nahodha Steven Gerrard kwa njia ya penati baada ya Luis Suarez kuangushwa katika eneo la hatari na Ryan Shawcross. 


Hata hivyo Stoke wakafanikiwa kusawazisha na baadaye kuandika bao la pili la uongozi kupitia kwa Jonathan Walters na kisha bao la kichwa la Kenwyne Jones.


Brendan Rodgers amekiri kikosi chake kuvurunda katika mchezo huo lakini pia akionekana kuhuzunishwa na aina ya magoli yaliyokuwa yakifungwa na kusema timu yake inapaswa kujifunza namna ya kulinda kama inataka kupata alama katika michezo ya ugenini.

“ulikuwa ni mwanzo mzuri kwetu kwa kupata goli la mapema kupitia njia ya penati, lakini tulishindwa kujilinda nadhani magoli yote matatu na makosa ya ulinzi, kiukweli hatukustahili chochote katika mchezo huu”

No comments:

Post a Comment