KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Friday, December 28, 2012

UKURASA WA HABARI ZA KIMATAIFA:Kagawa aleta matumaini sasa kuanzia benchi mchezo dhidi ya West Brom, Butland kumkimbiza Pepe Reina Liverpool, Birmingham yathibitisha na Meireles aleta kizaazaa Uturuki, apunguziwa adhabu ya michezo minne licha kumtemea mate usono mwamuzi.


Shinji Kagawa anatarajiwa kuwepo katika benchi la Manchester United Jumamosi katika mchezo dhidi ya West Brom.

Kiungo aliyejiunga na United akitokea Borussia Dortmund alikuwa nje ya uwanja tangu October 23 kutokana na kusumbuliwa na maumivu ya mguu mbayo aliyatapata katika mchezo wa vilabu bingwa ulaya(champions league) dhidi ya Braga.

Hapo kabla alitarajiwa kuwepo nje ya uwanja kwa wiki nne lakini kutokana na maumivu yeke kuendelea, akalazimika kuendelea kuuguza mguu kwa siku zaidi na tangu wakati huyo hajashuka dimbani.

Wakati hali ya mambo ikiwa hivyo, meneja Sir Alex Ferguson amesema kwakuwa mambo yanakwenda sawa kwasasa, anatarajia kuwa naye katika benchi jumamosi dhidi katika mchezo West Brom.

Mzee ferguson ameweka wazi kuwa anatarajia pia kuwa na Danny Welbeck pamoja naye Ashley Young hiyo jumamosi licha ya kwamba hakuwa tayari kuthibitisha kama Wayne Rooney atakuwepo ama la kama ilivyo kwa mlinzi Phil Jones ambaye ni dhihri shahiri atakosekana hiyo kesho.


Birmingham yathibitisha Liverpool kumtaka mlinda mlango wao Butland.
 Kaimu mwenyekiti wa Birmingham City Peter Pannu amethibitisha kuwa Liverpool iko katika mazungumzo na mlinda mlango Jack Butland.

Mlinda mlango hivi karibuni aliarifiwa kuwa anatakiwa na Liverpool ambayo inataka kupata mlinda mlango mbadala wa Pepe Reina.

Wakati huu ambapo Birmingham inayoshiriki ligi ya pili ya England ya Championship ikiwa katika hali mbaya kifedha tangu kushuka daraja kutoka ligi kuu “Premier League”, taarifa zinasema kuwa klabu hiyo inahangaika kusaka pesa kwa kuuza baadhi ya wachezaji wake wenye thamani ili kuweza kujinusuru na ukata huo.

Kaimu huyo wa mwenyekiti wa St. Andrews, Pannu, amepangusa aibu ya kuingiliwa na ukata na anathibitisha waziwazi kuwa jogoo wa England Liverpool ameonyesha nia ya kumtaka mlinda mlango wao kinda Butland na huenda akauzwa kujaribu kupunguza makali ya ukata na kusema kuwa ni Liverpool pekee ambayo imeonyesha nia mpaka sasa kumtaka mlinda mlango huyo wa kimataifa wa England.



Adhabu ya Meireles yapunguzwa mechi nne licha ya kumchafua kwa mate usoni mwamuzi.
 Kiungo wa Fenerbahce Raul Meireles amepunguziwa adhabu yake kutoka kusimama kwa michezo 11 na sasa kusaliwa na adhabu ya kusimama michezo 7 punguzo ambalo limefanywa na shirikisho la soka la Uturuki( Turkish Football Federation (TFF)) .

Kiungo huyo mreno mwenye umri wa miaka 29 hapo awali alipigwa adhabu ya kusimama michezo 11 kufuatia kushutumiwa kwa kosa la kumtea mate mwamuzi usoni baada ya mwamuzi huyo kumlima kadi nyekundu katika mchezo ambao Fenerbahce walipata kibano cha mabao 2-1 kutoka kwa Galatasaray.

Hata hivyo Meireles alikata rufaa ya kupinga adhabu hiyo na baadaye TFF iliona kweli ilikuwa vigumu kwa kiungo huyo wa zamani wa Chelsea kuweza kufanya kitendo hicho kwani kwa msaada ya video, alionekana akiongea mfululizo wakati akikabiliana na mwamuzi

Meireles, kwa nguvu zote alipinga adhabu hiyo na alikuwa akitaka adhabu hiyo kama si kuondoshwa basi ipunguzwe.

Alikaririwa akisema,
"hukumu imekwisha tolewa wakinishutumu mimi kufanya kitu ambacho sikufanya. Sikuwahi kumtemea mwamuzi mate.

Aidha klabu ya Galatasaray, imeshutumu maamuzi ya kupunguzwa kwa adhabu hiyo kulikofanywa na mahakama ya usuluhishi, taarifa ya klabu hiyo kupitia mtandao wa klabu imesomeka kwa kichwa cha habari “ ni aibu kwa soka la Uturuki ".

Taarifa hiyo imeendelea kusema

"kwa kumpunguzia adhabu Raul Meireles michezo minne ni kwamba kamati imepuuza ushahidi wa wazi'

"punguzo la adhabu ambayo imetokana na taarifa ya kweli ya mwamuzi, kushindwa kabisa, si tu kwa jamii nzima ya soka , lakini pia kwa fani nzima ya uamuzi. "

No comments:

Post a Comment