KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Thursday, January 3, 2013

UKURASA WA HABARI ZA KIMATAIFA: Baada ya kugongwa na kibonde QPR Benitez atetea uchaguzi wake. Asilimia 98% Demba ni wa Darajani. Siku moja baada ya kusajili Sturiidge Benitez amchimba mkwara mzito. QPR inamtaka Ben Haim na Liorente aanza mazungumzo na Juventus.

Kufuatia kugongwa na kibonde, Benitez atete uchaguzi wake wa wachezaji.
 Meneja wa Chelsea Rafael Benitez ametetea mabadiliko yake aliyoyafanya kuelekea kwenye mchezo dhidi ya QPR mchezo ambao Chelsea ilichapwa kwa bao 1-0 na timu ambayo iko mkiani katika msimamo wa ligi kuu ya England hapo jana.


Ryan Bertrand, Marko Marin, Victor Moses, Oscar na Ross Turnbull walikuwa ni miongoni mwa wachezaji waliongezwa na Benitez katika kikosi chake tofauti na kile kilicho ibuka na ushindi wa bao 2-1 dhidi ya 2-1 mwishoni mwa  juma.


Bernitez anasisitiza isingekuwa rahisi kuendelea kutumia wachezaji walewale waliotumika katika kipindi chote cha sikukuu na kudai kuwa Chelsea inapaswa kucheza mpira hata itawakosa watu kama Juan Mata na Eden Hazard.

"tulikuwa tunafanya vizuri na tulikuwa tunajiamini na mambo yalikwenda vizuri, tumebadili baadhi ya wachezaji lakini katika wachezaji wote hao tuliowabadili ni Marko Marin peke yake ndiye amekuwa hachezi mara kwa mara, Oscar alikuwa anacheza.

"ungeona baadhi ya wachezaji walivyokuwa wamechoka, hatukuwa na uwezo wa kumiliki mpira, hatukuwa tunapasiana mpira kwa uhakika na jazba ilikuwa inatawala, mwishowe tumefanya makosa na tumewapa nafasi, kulikuwa na mambo mengi hatuku yafanyia kazi.

"QPR walikuwa wamejipanga na walikuwa wanasubiria na walikuwa wanacheza mchezo wa kushambulia kwa ghafla(counter attack) na kutengeneza jambo ambalo limeleta tofauti mwisho wa mchezo.

"hatuwezi kutumia wachezaji walewale kila siku katika kila mchezo. Kama tunacheza na timu ambayo iko mkiani nyumbani unatakiwa kuwaamini wachezaji wako na ndivyo nilivyofanya"

Wakati Daniel Sturridge akikamilisha uhamisho wake wa kuelekea Liverpool, Fernando Torres alilazimika kuanza katika kikosi cha kwanza.

Benitez anaamini akimpata Demba Ba Chelsea italazimika kumpumzisha Torres.



 Siku moja baada ya kumsajili Sturridge, Rodgers amchimba mkwara.
 Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers amemuonya mchezaji wake mpya Daniel Sturridge ya kwamba yuko katika nafasi ya mwisho wanapo zungumzia klabu kubwa duniani hivyo anapaswa kukaza msuli.

Sturridge mwenye umri wa miaka 23, amekuwa ni mchezaji wa kwanza wa kusajiliwa na Rodgers mwezi January baada ya kukamilisha taratibu zote zilizo gharimu uhamisho wa pauni milioni £12 akitokea Chelsea na akisani kwa mkataba wa muda mrefu.

Lakini baada ya kupata nafasi ya kuanza katika jumla ya michezo 31 ya ligi katika kipindi cha miaka 3 akiwa na Chelsea na huku mara zote akipangwa kama winga ya kulia badala kucheza kama mshambuliaji wa kati, Rodgers anaamini mchezaji huyo wa kimataifa wa England anaweza kutumia vema fursa aliyoipata ya kucheza vizuri katika viunga vya Anfield.


"tumemchukua mchezaji ambaye anatakiwa kufanya kazi kama anataka kuwa ndani ya moja ya klabu kubwa duniani"

 Rodgers amesema

 "kama atataka kuwa katika kiwango bora, hii ni nafasi yake ya mwisho. Na hiyo ndiyo moja ya sababu"


QPR inamtaka Ben Haim
 Meneja wa Queens Park Rangers Harry Redknapp amethibtisha kuwa klabu yake imedhamiria kumpa mkataba Tal Ben Haim mpaka kumalizika kwa msimu.


Tal Ben Haim ameripotiwa kupokea pauni milioni £36,000 kwa wiki akiwa Portsmouth.

Ben Haim ambaye ana umri wa miaka  30, kwasasa ni mchezaji huru baada ya kuihama Portsmouth majira ya kiangazi na amekuwa akifanya mazoezi na QPR tangu mwanzoni mwa mwezi December.

Amenukuliwa Redknapp akisema baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Chelsea jana usiku.

"Tal amejituma sana katika kipindi cha mazoezi na tunaangalia kumpa mkataba mpaka mwisho wa msimu"

Nyota huyo wa kimataifa wa Israel alianza kugusa soka la England mwaka 2004 alipojiunga na Bolton, na baada ya hapo alijiunga na Chelsea, Manchester City, Sunderland na hivi karibuni akitokea Portsmouth.


Pardew: Demba Ba anaelekea Chelsea.
 Bosi wa Newcastle United Alan Pardew ana matumaini kuwa atazoea mazingira hata kama Demba Ba ataondoka ambapo inaarifiwa kuwa mshambuliaji huyo anaelekea kujiunga na Chelsea.

Demba mwenye umri wa  miaka 27, yuko katika mazungumzo na Chelsea juu ya kukamilisha taratibu za kujiunga Stamford Bridge baada ya makubaliano kufikiwa ya gharama za uhamisho ya pauni milioni £7 hapo jana.
Hata hivyo amesema atetereki na kuondoka kwa Ba kwa kuwa klabu hiyi ni kubwa na itaendelea kusonga mbele kama ilivyokuwa huko nyuma.
 

"tutasonga mbele hii ni klabu kubwa, ki ukweli klabu hii ni kubwa kuliko mchezaji yoyote yule"

Ba ameifungia Magpies magoli 29 katika jumla ya michezo 54 ndani ya kipindi cha miezi 18 alichoitumikia klabu hiyo ya kutoka pande za Tyneside.



 Juve katika mazungumzo na nyota wa Athletic Llorente
 Fernando Llorente anaelekea katika mazungumzo ya kutaka kujiunga na Juventus kwa uhamisho huru ambapo klabu yake ya sasa Athletic Bilbao ikitangaza kuwa mabingwa hao wa soka nchini italia wako pia katika mazungumzo ya kumsajili majira ya kiangazi.

Llorente mwenye umri wa miaka 27,ameweka wazi kuwa katika miezi ya hivi karibuni hakuwa na mpango wa kukubali mpango wowote na klabu hiyo toka pande za Basque, na kwamba kwasasa yuko huru kuongea na klabu yoyote itakayofaaa kwakuwa mkataba wake unakwenda kumalizika miezi sita ijayo.

Taarifa fupi iliyotolewa na mtandao wa Athletic imesema  "Juventus Football Club imekutana na Athletic Club hii leo kuzungumzia juu ya kumalizika kwa kipindi cha utumishi wa Fernando Llorente na klabu yetu June 30 2013, hivyo wameanza mazungumzo na mchezaji huyo ili kuwaongezea nguvu katika kikosi chao"

Wakati Juve wakikaribia kumnasa mshambuliaji huyo lakini bado kuna vilabu vingine vinavyomnyemelea kutoka ‘Premier League’ kama vile Arsenal, Tottenham na Liverpool na huenda vikawa pia ni vilabu mbadala endapo Juve watachemsha.

No comments:

Post a Comment