KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, January 6, 2013

UKURASA WA HABARI ZA KIMATAIFA: Ferguson hachoki kumfagilia Van Persie. Mourinho awatolea uvivu wachezaji wake na kusema hakuna mwenye namba ya kudumu Real na Vilanova arejea kibaruani.


 Sir Alex Ferguson amelikubali goli la kusawazisha la Manchester United baada ya kufanikiwa kulazimisha sare dhidi ya West Ham mchezo wa michuano ya FA.

Mabao mawili ya kichwa ya James Collins yaliyotokana na mpira wa krosi wa Joe Cole ambaye amerejea kwa washika nyundo akiwa amependeza katika rangi za jezi ya West Ham baada ya kuihama klabu hiyo karibu miaka 10 iliyopita na kuelekea Chelsea, yalikuwa kidogo yawape ushindi wa mabao 2-1.

Hata hivyo pasi murua ya mkongwe Ryan Giggs kwenda kwa Robin van Persie ambaye alimalizia kwa kufunga bao la kusawazisha liliiokoa United kutopoteza mchezo huo na kufanikiwa kupata sare ya mabao 2-2 katika dimba la Upton Park.

Meneja wa United Sir Alex Ferguson amevutiwa na bao zuri la Van Persie la kusawazisha akiwa katika msimu wake wa kwanza na klabu hiyo, akisema goli hilo lilikuwa safi na anatarajia mengi makubwa kutoka kwa mduchi huyo.

"yuko katika umri wa kupevuka sasa. Ameleta upevu katika safu ya ushambuliaji''



Mourinho awatolea uvivu wachezaji wake awapasha hakuna mwenye namba ya kudumu.
 Meneja wa Real Madrid Jose Mourinho amewatolea uvivu wachezaji wake na kuwaonya kuwa hakuna mtu mwenye nafasi ya kudumu katika kikosi cha Real.

Mlinda mlango wa Iker Casillas hakupangwa katika katika mchezo ambao Real Madrid ilipoteza kwa kufungwa magoli 3-2 na Malaga mwezi uliopita, jambo ambalo lilihatarisha kibarua cha kocha huyo.

Mabingwa hao wa Hispania hii leo wanakibarua dhidi ya Real Sociedad mchezo wao wa kwanza kwa mwaka huu wa 2013 na Mourinho akigomea kuweka wazi kama Casillas atakuwepo katika kikosi cha kwanza hii leo.

Alipoulizwa kuwa ni nani atakuwa golini katika mchezo wa leo Mourinho alijibu kwa dhihaka

"wachezaji wanajua nani atakuwa golini, unaweza kucheza leo lakini usiwepo katika mchezo wa jumatano wa Copa del Rey jumatano”

"kujiamini ni tafsiri ya kucheza vizuri, lakini kinachotakiwa ni kuwa katika kiwango cha ushindani na kuwa na uwiano sawa katika kila nafasi. Kuwa katika matumaini ya nafasi ya kudumu wakati mwingine si jambo jema"


Vilanova arejea kibaruani
 Kocha wa Barcelona  Tito Vilanova hii leo anarejea kuongoza kikosi cha timu yake dhidi ya Espanyol mchezo ambao ni wa timu zinazo toka katika eneo moja yaani ‘derby’.

Vilanova mwenye umri wa miaka 44, hivi karibuni alisumbuliwa na kansa ambayo iligundulika katika mwili wake mwaka 2011 ambapo kocha huyo raia wa Hiaspnaia alilazimika kufanyiwa upasuaji wa tezi ambapo kuelekea mwisho wa mwezi Rais wa Barca Sandro Rosell alisema kuwa kocha wake atarejea kazini katikati ya mwezi January.

Msaidizi wa Tito , Jordi Roura, amethibitisha kuwa Vilanova atakuwa kazini Camp Nou jumapili.

No comments:

Post a Comment