KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, January 6, 2013

KIMATAIFA ZAIDI: Montella afurahia ujio wa Rossi, Marseille inataka kumuuza Remy na Michu hangoki Swansea anasema Laudrup.


Vincenzo Montella ameelezea furaha yake baada ya kufanikisha usajili wa mshambuliaji mzaliwa wa New Jersey, Giuseppe Rossi akitokea Villarreal wakati huu ambapo dhamira ni kuhakikisha katika mwaka huu wa 2013 Fiorentina wanaanza na ushindi nyumbani dhidi ya Pescara.

Kwasasa wenyeji hao wa mji wa Viola wako katika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kuu ya nchini Italia Serie A, alama tisa nyuma ya vinara Juventus, na kocha anaamini kuwa usajili huo ambao kwao unatazamwa kama usajili mkubwa ambao utawawezesha kuelekea katika mwelekeo mzuri.

Rossi amekuwa nje ya uwanja tangu mwezi Oktoba mwaka 2011 kutokana na kuumia mfupa wa mguu anatarajiwa kurejea dimbani mwezi March.


Marseille iko tayari kumuuza  Remy.
 Mkurugenzi wa michezo wa Olympique de Marseille, Jose Anigo amesema klabu yake iko tayari kumuuza Loic Remy katika kipindi hiki cha majira ya baridi endapo bei ya thamani ya mchezaji huyo itafikiwa.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ufaransa amekuwa akihusishwa kwa muda mrefu na kuihama Marseille, na lengo lake likiwa ni kutaka kuelekea katika soka la England.

Newcastle inaaminika kuwa ndio kinara wa mbio hizo za kupata saini ya mshambuliaji huyo.

Anigo, ambaye ndiye kiongozi wa usajili katika klabu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya nchini Ufaransa ‘Ligue 1’ amesema Remy huenda akaondoka Stade Velodrome mwezi huu endapo pesa yenye thamani ya mchezaji huyo itafikiwa.

Bosi wa Swansea Laudrup anasema Michu hataondoka mwezi huu wa January
 Meneja wa Swansea City Michael Laudrup amedai kuwa mshambuliaji wake Michu hawezi kuondoka katika dirisha hili la usajili la mwezi wa January.

Mhispania huyo amekuwa katika kiwango cha juu katika safu ya usahmbuliaji ya klabu hiyo tangu kujiunga nayo kwa uhamisho wa pauni milioni mbili akitokea Rayo Vallecano msimu uliopita na msimu huu akiwa amesha pachika wavuni jumla ya mabao 13 katika jumla ya michezo 22  msimu huu.

Timu mbili za nchini Russian, Zenit St Petersburg na Anzhi Makhachkhala zimeripotiwa kutaka kumsajili mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 26, lakini bosi huyo wa Swansea amesisitiza kuwa mshambuliaji huyo ataendelea kusalia Liberty Stadium mwezi huu.

No comments:

Post a Comment