KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, March 31, 2013

HABARI ZA MICHEZO ZA KIMATAIFA: Rafael Benitez kwa kuwaweka benchi akina Luiz na Cole nje na kupokea kichapo. Martin O'Neill afukuzwa kazi Sunderland. West Ham imenogewa na mkopo wa Andy Carroll . David Beckham anafikira kuongeza msimu PSG. Liverpool yaibabua Aston villa na Mattsson aikimbia kazi ya kufundisha Sierra Leone.




Rafael Benitez amejitetea juu ya maamuzi yake ya kufanya mabadiliko madlikom kwa wachezaji saba katika mchezo wa jana ambao Chelsea ilichapwa bao 2-1 na Southampton wakati huu ambapo wanaelekea katika mchezo wao wa robo fainali ya michuano ya FA hapo kesho jumatatu dhidi ya Manchester United.

Walinzi wa David Luiz na Ashley Cole pamoja na kiungo Eden Hazard hawakuwepo katika kikosi ambacho kiliishuhudia hapo jana Chelsea ikidondoka kutoka katika nafasi ya tatu mpaka ya nne ya msimamo wa ligi kuu ya soka England.

Amenuliwa bosi huyo wa muda akisema

"tumefanya hivyo ili kuelewa kikosi na kukijenga"

"Hatukuwa na namna nyingine ya kufanya katika baadhi ya nafasi, tulikuwa na wachezaji hao tuliokuwa nao"

Gary Cahill hakuwepo katika mchezo huo dhidi ya Southampton kwasababu ya maumivu ya mguu kama ilivyokuwa kwa Juan Mata ambaye naye alikuwa ni mgonjwa.

Benitez amesema

"lazima tukabiliane na hali katika kila mchezo ni jambo muhimu sana na tulidhani kwa kuwatumia wachezaji hao mambo yangekuwa mazuri.

Licha ya kwamba huo ulikuwa ni mchezo wa tatu mfululizo kwa Chelsea kufungwa ugenini katika ligi ambao umewapandisha juu Tottenham, bosi huyo mhispania amesisitiza kuwa kikosi chake kilikuwa vizuri.


 MICHEZO MUHIMU KWA CHELSEA


1 April: H v Man Utd (FA Cup quarter-final replay)

4 April: H v Rubin Kazan (Europa League quarter-final first leg)

7 April: H v Sunderland (league)

11 April: A v Rubin Kazan (Europa League quarter-final second leg)



Martin O'Neill afukuzwa kazi Sunderland

Sunderland iliyo katika nafasi ya hatari ya kushuka daraja imemfukuza kazi meneja wake Martin O'Neill kufuatia matokeo mabaya ya michezo mbalimbali ya ligi kuu ya nchini England.

Paka mweusi ana alama moja tu juu ya msatari wa kushuka daraja relegation zone ya Premier League relegation ikiwa pia imesaliwa na michezo saba jana ilipokea kichapo kingine cha bao 1-0 kutoka kwa Manchester United.

Sunderland haijashinda katika michezo nane mfululizo ya ligi kuu na katika jumla ya michezo yote hiyo imeambulia alama tatu.

Taarifa ya klabu hiyo imesema kuwa maamuzi ya nani atarithi mikoba ya O'Neill's yatafanyika katika siku chache zijazo.

Paolo Di Canio mwenye umri wa miaka 44, anatajwa kuwa mrithi wake.

Meneja huyo wa zamani wa West Ham United aliondoka katika klabu ya League One ya Swindon mwezi Februari, ambayo ilikuwa ni klabu yake ya kwanza kama meneja.

Pia meneja wa zamani wa timu ya taifa ya England Steve McClaren, ambaye naye aliondoka kibaruani FC Twente mwezi February, anahusishwa na kuchukua nafasi hiyo ya kazi.

Majina mengine ni pamoja na meneja wa zamamni waklabu za Queens Park Rangers na Manchester City  Mark Hughes na Roberto Di Matteo ambaye alitwaa taji la mabingwa Ulaya na michuano ya FA akiwa kama meneja wa muda wa Chelsea msimu uliopita.

Mchezaji wa zamani wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer, ambaye kwasasa yuko katika klabu ya nchini Norway ya Molde, pia anahusishwa na kazi hiyo kama ilivyo kwa bosi wa Brighton, Gus Poyet.


West Ham imenogewa na mkopo wa Andy Carroll
 Meneja wa West Ham Sam Allardyce ana imani kuwa atambakisha mshambuliaji wake aliye kwa mkopo katika klabu hiyo yenye maskani yake Upton Park Andy Carroll mpaka msimu ujao.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka  24 alifunga magoli mawili –katika mchezo dhidi ya West Brom na taarifa zinasema kuwa mshambuliaji huyo yuko mbioni kurejea Liverpool wakati wa kiangazi baada ya msimu mrefu wa mkopo.
Alipoulizwa juu ya mfungaji huyo wa zamani wa Newcastle kusalia , Allardyce alijibu kuwa siku zote amekuwa katika kuamini hilo linawezekana.
"tutaangalia mwishoni mwa msimu na tutaangali namna ya kufanya mazungumzo"
Carroll alijiunga na Liverpool kwa uhamisho wa rekodi ya klabu hiyo wa pauni milioni 35 mwezi januari 2011.
Alisajiliwa ili kuziba pengo la Fernando Torres kufuatia mhispania huyo kuhamia Chelsea kwa uhamisho wa pauni milioni 50 lakini hata hivyo Carrol alishindwa kufanya vema Anfield na tangu wakati huo akapoteza hata nafasi yake katika kikosi cha timu ya taifa ya England.
Mshambuliaji huyo mrefu wa futi sita alitumikia michezo miwili tu Liverpool chini ya meneja Brendan Rodgers msimu huu kabla ya kujiunga na washika nyundo mwezi August.
 

David Beckham anafikira kuongeza msimu PSG
 David Beckham ameweka wazi amedhamiria kuongeza muda wake wa kusalia katika klabu ya Paris St-Germain ya nchini Ufaranza mpaka msimu ujao.

Nahodha huyo wa zamani wa timu ya taifa ya England baada ya kumaliza makataba wake katika klabu ya Los Angeles Galax alikuwa na ofa za vilabu kumi na moja kwa mkataba wa miezi mitano lakini chaguo lake lilikuwa ni PSG.

Amenukuliwa na Le Parisien akiuliza

"Ni nani asiyependa kuwepo sehemu kama hii? Ni sehemu ambayo ambayo kila mtu anataka kuwepo.".

Kocha wa PSG cCarlo Ancelotti amesema kuwa

"ningependa kuona David Beckham akiongeza mkataba"

Ndani ya kipindi alichokuwepo Paris, Beckham amechangia kuivusha PSG ikitinga robo fainali ya vilabu bingwa Ulaya na sasa ikisubiri mchezo dhidi ya Barcelona na wakati huo huo PSG ikisalia katika kilele cha msimamo wa ligi kuu nchini Ufaransa Ligue 1.

Beckham ametoa kauli hiyo Ijumaa baada ya mchezo dhidi ya mabingwa watetezi wa ligi ya nchini humo Montpellier ambapo walichomoza na ushindi wa bao 1-0 ambapo aliingia dakika 18 za mwisho katika mchezo huo.

Anatarajiwa kuwa msaada mkubwa katika mchezo dhidi ya Barca akitoa mchango kama mchezaji mzoefu.



Liverpool yaibabua Aston villa


Aston Villa imeshindwa kujiondoa katika eneo la hatari la uwezekano wa kushuka daraja katika ligi ligi kuu ya chini England ‘Premier League ‘ kufuatia Liverpool ilitokea nyuma kimatokeo kuibuka na ushindia wa mabao 2-1 mchezo uliofanyika Villa Park.

Kikosi cha Paul Lambert kilianza kuandika bao la uongozi kufuatia mpira wa Gabriel Agbonlahor kumkuta Christian Benteke aliyeandika bao hilo.

Liverpool ilisawazisha muda mfupi baada ya mpira kuanza kati pale ambapo Jordan Henderson alipo uchopu mpira uliompita mlinda mlango Brad Guzan.

Naye Steven Gerrard aliandika bao la pili kwa njia ya penati kufuatia Nathan Baker kumuangusha Luis Suarez katika eneo la hatari.



Mattsson aikimbia kazi ya kufundisha Sierra Leone.
 Kocha wa timu ya taifa ya Sierra Leone Lars Olof Mattsson ameachana na kazi ya kuifundisha timu ya taifa ya nchi hiyo baada ya miaka miwili ya kuifundisha timu hiyo lakini hata hivyo kuna habari za kutatanisha juu ya kujiuzulu kwake.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 58 raia wa Sweden amedai kuwa tayari alikwisha kuwaandikia barua chama cha soka cha nchi hiyo (SLFA) na nyingine kwenda kwa waziri wa michezo. Lakini hata hivyo SLFA na wizara wamekanusha kupokea barua ya Mattsson
 Msemaji wa SLFA Sorie Ibrahim amenukuliwa akisema
 “kama anataka kujiuzulu kazi alipaswa kuwasiliana na sisi kwa kuwa ni mwajiri wake na kwenda kwenye vyombo vya habari vya Sweden”
"Bado tunachukulia kocha Mattsson kuwa ni kocha wetu nab ado hatuja pokea barua yake. Tumesikia taarifa hizi kupitia vyombo vya habari vya Sweden”
Mattsson alielezea matatizo katika timu ya taifa ya Siera Lione Leone Stars ambayo ameiongoza mpaka mwishoni mwa juma ambapo walifungwa na Tunisia mabao 2-1 mchezo wa kufuzu kombe la dunia, pia ameelezea kuwa hana mkataba na SLFA.

No comments:

Post a Comment