KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Tuesday, April 9, 2013

Bellew kuzipiga na Chilemba mchezo wa kumaliza ubishi likiwa ni pambano la utangulizi la Froch na Kessler.

Gutted: Tony Bellew felt he deserved to win his first fight with Isaac Chilemba
Tony Bellew anadhani alistahili ushindi katika mchezo wake dhidi ya Isaac Chilemba.

Mchezo wa marudiano wa masumbwi baina ya Tony Bellew dhidi ya Isaac Chilemba utachezwa Mei 25 katika ukumbi wa  O2 Arena likiwa ni pambano la utangulizi la Carl Froch dhidi ya Mikkel Kessler.

Pambano hilo lenye mvuto mkubwa la jijini Liverpool la uzito mwepesi wa juu lilimalizika kwa sare mwezi uliopita.

Taarifa zinasema kuwa mshindi wa pambano hilo atakuwa akimsubiri mshindi wa pambano la kusaka mshindi la WBC baina ya Chad Dawson dhidi ya Adonis Stevenson litakalochezwa Juni 8.

Mtayarishaji Eddie Hearn ameweka wazi hilo kuwa mabondia wote wako tayari kwa mchezo wa marudiano haraka iwezekenavyo.

Amenukuliwa akisema. 
 'Hakukuwa na mshindi na sisi tunataka mshindi '

'Watu wengi walidhani Tony alishinda na wengine walidhani Chilemba alishinda katika pambano lililopita. Ni pambano ambalo inabidi kuyasahau yaliyopita'
Draw: Bellew took his foot off the gas after the opening rounds
Wakati huohuo mpinzani wa George Groves ambaye atacheza pambano lingine la utangulizi usiku huo atatangazwa wiki hii.

No comments:

Post a Comment