KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, July 27, 2013

Internacional ya Brazil yawaambaia Spurs na Southampton kama wana mtaka mshambuliaji wake Leandro Damiao itawagharimu pauni milioni £22.

Spurs and Saints told to bid £22m for Damiao
Leandro Damiao si wa bei ndogo kihivyo.
Klabu ya soka ya Internacional ya nchini Brazil imeviambia vilabu vya Tottenham na Southampton kuwa watatakiwa angalu kulipa pauni milioni £22 ili kumsajili mshambuliaji wake Leandro Damiao.

Vilabu vyote Spurs na Southamton vimekuwa vikifuatialia saini ya Damiao kwa udi na uvumba kiangazi hii baada ya mshambuliaji huyo kutamka kuwa anapenda kucheza katika ligi kuu ya soka nchini England Premier League.

Hata hivyo mkurugenzi wa Internacional Marcelo Medeiros amevionya vilabu hivyo vinavyo muwania Damiao wasielekee kwao wakidhani kuwa mshambuliaji huyo ni wa bei rahisi.

Amenukuliwa na gazeti la Globo akisema
‘Bei ya Damiao ni pauni milioni £22million kama kuna klabu ambayo inamtaka Damiao, hiyo ndiyo bei yake.’
Brazil's Leandro Damiao (R) vies for the
Damiao anatamani soka ya England.
 
Tottenham wanamtazama mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 24 kama mbadala wa Roberto Soldado endapo watamkosa, ambapo meneja Andre Villas-Boas anasema alikaribia kumsajili mshambuliaji huyo wakati wa dirisha la mwezi Januari na kusema ataendelea kumfuatialia.

Tayari Dejan Lovren na Victor Wanyama wameshatua kwa hela nyingi lakini inaarifiwa kuwa Damiao huenda akawa na gharama ya juu kuliko wote.
Napoli iliweka wazi mapema mwezi huu kuwa wanamtaka mshambuliaji huyo lakini walibadilisha nia na kuelekeza nguvu kwa Gonzalo Higuain na mshambuliaji wa Porto Jackson Martinez.

No comments:

Post a Comment