KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, August 26, 2013

UKURASA WA KIMATAIFA:Kocha wa Togo Didier Six kusalia katika benchi mpaka mchezo dhidi ya DR Congo, Cameroon imemuita mlinda mlango Idriss Kameni kuelekea katika mchezo dhidi ya Libya, Gareth Bale: Spurs inafikiria ofa pinzani na ile ya Real Madrid huenda ikawa ni Manchester United NA Arsene Wenger nataka mchezaji 'special'.


Kocha wa Togo Didier Six kusalia katika benchi mpaka mchezo dhidi ya DR Congo
 Didier Six amekubali kusalia katika benchi la ufundi la Togo katika mchezo wao wa kusaka nafasi ya kucheza kombe  la dunia dhidi ya DR Congo mwezi September kabla ya kujiuzulu nafasi yake ya ukocha.
Mfaransa huyo mwezi wa juni alikaririwa akisema anataka kungatuka katika nafasi yake kutokana na kutokuwa na maelewano mazuri shirikisho la soka la nchi ya Togo (TFF) juu ya gharama na kwamba asingeweza kurejea mjini Lome.
Lakini Six na TFF hatimaye wamemaliza mzozo baina yao na kufikia katika makubalino kuwa kocha huyo mwenye umri wa miaka 58 kuendelea katika nafasi yake hiyo mpaka katika mchezo wa mwisho wa kundi I wa kusaka nafasi ya kucheza kombe la dunia.
Togo wako katika mkia wa kundi hilo ilhali DR Congo wakishika nafasi ya tatu huku kila timu ikiwa imeshindwa kufuzu kueleka katika michezo ya mwisho ya mtoano ambayo itaamua mustakabi wa nani kafuzu na nani kashindwa kufanya hivyo.
Mchezo baina ya timu zote mbili umekosa msisimko kutokana na msimamo wa kundi kwani timu hazina nafasi na hivyo utakuwa ni mchezo wa kukamilisha ratiba tu na utakuwa unakamilisha kipindi cha miaka miwili ya utumishi wa kocha huyo ndani ya TFF.
Msemaji wa TFF Herve Agbodan amesema

"Kocha Didier Six amerejea kutoka Ulaya lakini amewasilisha orodha ya wachezaji atakao watumia dhidi ya DR Congo na amekubali kuwepo katika benchi katika mchezo wa mwisho.
Togo inatarajiwa kutangaza kikosi chake rasmi wiki ijayo na taarifa za fununu zinasema kocha huyo amewaacha wachezaji muhimu kama mshambuliaji Emmanuel Adebayor, mlinda mlango Agassa Kossi kiungo mchezeshaji Alexis Romao.

 Cameroon imemuita mlinda mlango Idriss Kameni kuelekea katika mchezo dhidi ya Libya.
Kocha wa kikosi cha timu ya taifa ya Cameroon Volker Finke amemuita tena mlinda mlango Idriss Carlos Kameni katika kikosi chake cha wachezaji 25 kitakacho kabiliana na Libya mwezi ujao ambao ni mchezo muhimu wa kuwania kufuzu kwa fainali za kombe la dunia.
Cameroon inaongoza kundi ‘I’ kwa alama moja mbele ya Libya.
Finke ameamua kumwita tena mlinda mlango mzoefu Kameni, ambaye alishiriki katika michuano miwili ya kombe la dunia iliyopia na michuano mara tano ya fainali za michuano ya mataifa ya Afrika.
Mlinda mlango huyo wa Malaga kwa mara ya mwisho kuitumikia timu ya taifa ilikuwa mwezi Septemba mwaka 2012 pale Cameroon ilipoichapwa bao 2-0 na Cape Verde katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika.
Pia kocha huyo amemrejesha kikosini mshambuliaji Idrissou Mohammadou, ambaye ameifungia magoli sita katika michezo sita ya klabu yake ya FC Kaiserslautern ya nchini Ujerumani.
Mchezo wa mwisho kuichezea Cameroon ni mchezo wa pili wa marudiano dhidi ya Cape Verde uliopigwa mjini Yaounde ambao licha ya Cameroon kushinda kwa mabao 2-1 lakini bado waliondolewa katika kinyanganyiro cha fainali za mataifa ya Afrika.
Gaetang Bong na Jean Armel Kana Biyik wote wamerejeshwa kikosini lakini Fabric Olinga ametupwa katika orodha ya wachezaji wa pembeni.
Katika safu ya ushambuliaji , Cameroon itakuwa ikiwategemea Samuel Eto'o na Choupo Moting.
Finke hajamwita mchezaji hata mmoja kutoka katika ligi ya nyumbani.
Kikosi kamili
Walinda mlango : Idriss Carlos Kameni (Malaga, Spain), Charles Itandje (Konyaspor, Turkey), Sammy Ndjock (Antalyaspor, Turkey).
Walinzi : Allan Nyom (Grenada, Spain), Aurelien Chedjou (Galatasaray, Turkey), Benoit Angbwa (Kryla Sovetov Samara, Russia), Dany Nounkeu (Galatasaray, Turkey), Nicolas Nkoulou (Marseille, France), Gaetan Bong (Olympiakos, Greece), Jean-Armel Kana-Biyik (Rennes, France), Benoit Assou-Ekotto (Tottenham, England).
Viungo : Stephan Mbia (Queens Park Rangers, England), Eyong Enoh (Ajax Amsterdam, Ireland), Jean II Makoun (Rennes, France), Joel Matip (Schalke 04, Germany), Raoul Cedric Loe (Osasuna, Spain), Landry Nguemo (Bordeaux, France).
Washambuliaji : Samuel Eto'o (Anzhi Makhachkala, Russia), Achille Webo (Fenerbahce, Turkey), Aboubakar Oumarou (Vojvodina Novi Sad, Serbia), Eric-Maxim Choupo Moting (Mayence, Germany), Jacques Zoua (Hambourg, Germany), Benjamin Moukandjo (Nancy, France), Jean-Marie Dongou (FC Barcelone, Spain).

Gareth Bale: Spurs inafikiria ofa pinzani na ile ya Real Madrid huenda ikawa ni Manchester United
Tottenham imepokea ofa mbili zaidi za rekodi ya usajili ya dunia kutoka katika klabu ya Real Madrid ya pauni milioni £86 ikimuhusisha Gareth Bale.
Madrid moja ya klabu kigogo cha nchini Hispania iko katika nafasi ya juu yenye lengo la kumsajili mshambuliaji huyo wa Wells mwenye umri wa miaka 24, lakini bado klabu yake ya Spurs inasema hakuna makubaliano yaliyofikiwa na Real.
Ombi linguine la pili bado halijafahamika lakini Manchester United imekuwa ikihusishwa na ofa hiyo majira haya ya kiangazi.
Wakati huohuo Spurs imeiambia klabu ya Chelsea kuwa inataka kumsajili mchezaji kutoka katika klabu hiyo kwa lengo la kuziba nafasi ya Bale.
Walikuwa karibu kumsajili winga wa kibrazil Willian kama mbadala wa Bale wiki iliyopita kabla ya pigo la kunyaka saini yake.
Bale, aliyejiunga na Spurs kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni £10 akitokea katika klabu ya Southampton 2007, alitajwa kuwa mchezaji wa mwaka katika maeneo mawili ya mchezaji bora wa kulipwa na mchezaji bora chama cha waandishi wa habarimsimu uliopita baada ya kuwafungia vijana wa White Hart Lane jumla ya mabao 26.
Madrid tayari imeshatumia jumla ya pauni milioni £50 majira haya ya kiangazi kwa kuwasajili viungo Asier Illarramendi kutoka katika klabu ya Real Sociedad Isco kutoka Malaga kwa ada za uhamisho za pauni milioni £34 na £23.

Arsene Wenger nataka mchezaji 'special'.
 Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amesisitiza kuwa atamchukua mchezaji muhimu tu kuelekea katika klabu yake ya Arsenal, ikiwa imesalia wiko moja kabla ya dirisha la usajili halijafungwa
Arsenal kwasasa bado inaendelea na mawindo ya wakali watatu , wawili kutoka katika klabu ya Real Madrid ambao ni Karim Benzema na Angel Di Maria, pamoja na Yahan Cabaye wa Newcastle United.
Amesema hayo baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Fulham Jumamosi akisema "They are special and if I want to add something it has to be special."
Katika miezi ya hivi karibuni kikosi hicho toka pande za London ya kaskazini kilishindwa kufanya uhamisho wa kumchukua mshambuliaji Luis Suarez wa Liverpool , pamoja na kushuhudia ofa yao ya pauni milioni £10 ya kumtaka Cabaye ikitupiliwa mbali huku pia wakihusishwa na mpango wa kutaka huduma ya mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney na  Gonzalo Higuain, ambaye alikwenda kujiunga na Napoli akitokea katika klabu ya Madrid.
Mathieu Flamini inaaminika yuko katika mazungumzo juu ya kurejea ndani ya klabu hiyo kwa uhamisho huru na hapo kabla alikuwa akifanya mazoezi na washika mitutu hao wa London katika kipindi chote cha kiangazi.
Kiungo huyo aliihama Arsenal na kujiunga na AC Milan ya Italia mwaka 2008.

No comments:

Post a Comment