KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, September 2, 2013

Mbio za magari: Rais Jean Todt apata mpinzani kuelekea uchaguzi mwezi Disemba

Rais wa shirika linaloongoza mchezo wa mbio za magari duniani FIA Jean Todt, atakabiliwa na upinzani mkubwa wa kutetea nafasi yake ya Urais mwezi Desemba, baada ya David Ward kutangaza kugombea nafasi hiyo.

David Ward ambaye ni mkurugenzi mkuu wa shirika huru la hisani la Taasisi ya FIA, amejiuzulu nafasi yake hiyo baada ya miaka 12, ili apambane dhidi ya Todt. Ward mwenye umri wa miaka 56, alisema kipindi cha uchaguzi kinaanza mwezi huu wa Septemba, na kwa hivyo ilikuwa muhimu kwake kuwafikia wanachama wa FIA ili aweze kupata uteuzi.

Todt alimrithi Max Mosley kama rais wa FIA mwaka 2009, baada ya kumshinda Ari Vatanen katika uchaguzi wa baraza kuu ya FIA, lakini Mfaransa huyo bado hajathibitisha iwapo anataka kugombea muhula wa pili baada ya muhula wake wa sasa kukamilika mwishoni mwa mwaka huu. Ward anajivunia mtandao mkubwa wa kisiasa ndani ya FIA, unaotokana na nafasi yake ya zamani kama msaidizi wa Mosley.

Kimi Raikkonen. Kimi Raikkonen.

Lotus yambembeleza Kimi Raikonnen

Na timu ya mashindano ya Lotus inafanya kila jitihada kumshawishi dereva Kimi Raikonnen abaki katika timu hiyo msimu ujao, mkuu wa timu hiyo yenye makao yake nchini Uingereza Eric Boullier amesema. Kumekuwa na minon'gono ya hapa na pale kuhusu mustakabali wa dereva huyo, raia wa Finnland mwenye umri wa miaka 33.
Wakati akisema anatumaini kuwa bingwa huyo wa dunia wa mwaka 2007 ataendelea kuwepo katika timu ya Lotus, Boullier alikri kuwa yapo masuala kadhaa yasiyopatiwa ufumbuzi, ambayo yanapaswa kushughulikiwa kabla ya kusaini mkataba mpya. Raikonnen yuko pointi 63 nyuma ya dereva anaeongoza katika ubingwa, Sebastian Vettel kutoka Ujerumani.

No comments:

Post a Comment