KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, September 28, 2013

MESSI AVUNJA REKODI NYINGINE YA MABAO NDANI YA BARCELONA LEO SOMA...............



Lionel Messi sasa amekuwa ndiye mfungaji kinara mwenye magoli mengi zidi katika michezo ya kimashindano kuliko mchezaji mwingine yoyote katika historia ya klabu ya Real Madrid baada ya kumzidi mkongwe wa zamani wa klabu hiyi  maarufu kama 'Blancos' huyu si mwingine ni Raul baada ya kufunga magoli hii leo.

Mshambuiliaji huyo wa kimataifa wa Argentina alipiga bao la pili la Barcelona katika mchezo wa ligi Jumanne pale walipoibuka na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Real Sociedad mchezo wa ligi ya Hispania 'La Liga' ambapo alilingana na Raul kwa kufunga goli la 323 lakini goli lake safi la leo dhidi ya Almeria lilitosha kumpiku mshambuliaji wa zamani Raul kwa kufunga magoli ya kimashindano.

Messi amefunga sasa jumla ya magoli 324 ya kimashindano katika jumla ya michezo 388 aliyochezea Camp Nou akiwa bado ana umri wa miaka 26.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Argentina, kwasasa ana magoli 62 ya michuano ya Champions League akiwa nyuma ya Raul mwenye rekodi ya magoli 71 ya michuano ya vilabu Ulaya.

Mabao hayo 323 ya Raul aliyo ifungia Real Madrid ni katika jumla ya michezo 741 ndani ya misimu 16 ndani ya Santiago Bernabeu. Messi mwenye magoli 324 ana kampeni 10 ndani ya klabu hiyo ya Katalunya.

No comments:

Post a Comment