KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Saturday, October 26, 2013

Arsene Wenger alalamikia kadi nyekundu ya moja kwa moja ya Mikel Arteta.


Meneja wa Arsene Wenger wa Arsenal amemjia juu mwamuzi Chris Foy kwa kumtoa nje ya uwanja Mikel Arteta katika mchezo wao wa leo dhidi ya Crystal Palace, akisisitiza kuwa alifanya maamuzi ya uongo.
Arteta alitolewa nje ya uwanja kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja baada ya kumfanyia madhambi mshambuliaji wa zamani wa klabu hiyo Maroune Chamakh wakati akikaribia lango la washika mitutu.
Wenger amesema maamuzi ya Foy ya kumtoa nje Arteta yalikuwa si sahihi.
Crystal Palace v Arsenal - Barclays Premier League
Arteta akitolewa nje baada ya kumkabili Maroune Chamakh
‘Arteta hakuwa mtu wa mwisho na ilikuwa ni fursa ya mshambuliaji kufunga. Chamakh alikuwa mbali na goli na faulo ilikuwepo ndiyo.’

No comments:

Post a Comment