KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, October 21, 2013

Mjumbe wa fifa aliyefungiwa Mnigeria Adamu amaliza adhabu.

Kifungo cha mjumbe wa zamani wa shirikisho la soka duniani Fifa Amos Adamu cha miaka mitatu sasa kimemalizika.
Mnigeria huyo alihukumiwa kwa kifungo hicho baada ya kudaiwa kudai fedha kwa ajili ya kulipa fadhila ya kupiga kura kwa wenyeji wa kombe la dunia katika fainali za michuano ya 2018 na 2022.
Alionekana pichani akidai dolari za kimarekani $800,000 kabla ya kuondolewa katika zoezi la upigaji kura la mwaka 2010.

Adamu, ambaye kwasasa yuko huru kufanya kazi za mpira wa miguu baada ya adhabu yake kukamilika hapo jana amekaririwa akisema
"Namshukuru mungu adhabu imkwisha . Sina kinyongo na mtu."
Sasa ni mtu mwingine tena mwerevu kuliko hapo kabla
Amos Adamu
Skendo hiyo ya rushwa na kifungo cha miaka mitatu kwa Adamu ambayo pia iliwakumba wajumbe wengine watano ambao walisimamishwa katika zaozi la upigaji kura ambazo ziliamua Russia kuwa wenyeji wa fainali za kombe la dunia mwaka 2018 nao Qatar ikiamualiwa kuandaa fainali za 2022.

No comments:

Post a Comment