KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Monday, October 28, 2013

UCHAGUZI WA TFF: MATUKIO ZAIDI KATIKA PICHA

Rais Mpya Jamal Malinzi (kulia) akipokea katiba ya TFF toka kwa Rais anayemaliza muda wake Leodgar Tenga
Hapa akikabidhiwa mpira.
Kamati ya uchaguzi ikikamilisha kazi
Uongozi mpya wa TFF
Ayub Nyenze akiwa ameshikiliwa na madaktari baada ya presha kupanda kwa furaha ya ushindi
Athuman Nyamlani akiondoka ukumbini mapema saa tatu baada ya kusikia fununu kuwa kashindwa
Wapambe wa Malinzi wakipongezana baada ya kusikia ushindi wa Malinzi
Wajumbe wakifuatilia matokeo ukumbini hapo ni Linna Kessi mjumbe mpya na Simon Nyala aliye angushwa


Tenga akiwa na Mamelod (katikati)  na Tandau
Hapa wajumbe wamechoka hadi wanasinzia
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya uchaguzi mpya
KATIKA kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu wa TFF, uliofanyika jana na kumalizika alfajiri ya leo, Jamal Emil Malinzi,amefanikiwa kuibuka kidedea na kuwa Rais mpya wa Shirikisho hilo baada ya kuibuka na jumla ya Kura, 72 dhidi ya 52 za mpinzani wake Athumani Jumanne Nyamlani.

Katika uchaguzi huo uliofanyika kwenye ukumbi wa NSSF Water Front, Dar es Salaam, Walace Karia alifanikiwa kushinda nafasi ya Makamu wa Rais kwa kupata jumla ya kura 67 akiwashinda Nassib Ramadhani aliyeibuka na kura 52 na Imani Madega, aliyepata 6. 

Katika nafasi za Ujumbe; Kanda ya 13; kiungo wa zamani wa Simba SC Wilfred Kidau amepata kura 60 na kuwashinda Muhsin Said aliyepata kura 50, Omar Abdulkadir, kura 10 na Alex Kabuzelia kura nne.
Kanda 12; Khalid Mohamed Abdallah amepata kura 69 na kumshinda Davisa Mosha aliyepata kura 54.

Kanda ya 11 Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ amepata kura 78 na kuwashinda Riziki Majala aliyepata kura tano, Twahir Njoki kura mbili, Juma Pinto kura 26 na Farid Mbaraka kura 14.
Aliyeshinda Kanda ya 10 ni Hussein Mwamba aliyepata kura 63, huku Charles Komba akipata kura nne na Stewart Nasima kura 58.

Kanda ya 9, Othman Kambi aliyepata kura 84 ndiye aliyewashinda wapinzani wake, Francis Bulame aliyepata kura kura 30 na James.

Baada ya kutangazwa Jamali alitoa shukurani na kuvunja kamati zote za TFF na kuwasamehe  waamuzi wote waliofungiwa kwa makosa ya kawaida isipokuwa wale waliofungiwa kwa makosa ya rushwa. 

No comments:

Post a Comment