Kikosi cha Löw kinamjumuisha kipa wa Borussia Dortmund Roman Weidenfeller. |
Kocha wa timu ya taifa ya Ujerumani Joachim Löw amemwita kikosini Roman
Weidenfeller kwa mara ya kwanza.
Mlinda lango huyo wa Borussia Dortmund
ataichezea Ujerumani mechi za kirafiki dhidi ya Uingereza na Italia.
Löw, amesema Weidenfeller mwenye umri wa miaka 33 hatimaye ameanza
kupata fursa yake ya kuichezea timu ya taifa.
Amesema mchezo wake katika
klabu ya Dortmund ambao sasa iko katika nafasi ya pili katika msimamo
wa ligi, umekuwa mzuri kiasi cha kutoweza kupuuza.
Ijapokuwa mlinda lango wa Bayern Munich Manuel Neuer anasaliwa kuwa kipa
nambari moja wa Ujerumani, Löw amesema sasa Weidenfeller ana jukumu la
kupigania nafasi yake ya kuwa mlinda lango wa akiba au nambari tatu
katika timu ya taifa kabla ya fainali ya kombe la dunia nchini Brazil
hapo mwakani.
Pia amemwita kikosini mshambuliaji Miroslav Klose baada ya kupona jeraha,
lakini kiungo Bastian Schweinsteiger bado ataendelea kuwa nje ya kikosi kipindi hiki.
Klose, mchezaji
mwenye uzoefu mkubwa mwenye umri wa miaka 35 wa klabu ya Lazio, anarejea
kikosini baada ya kuachwa nje katika mechi za kufuzu kwa dimba la dunia
mwezi uliopita, dhidi ya Jamhuri ya Czech na Sweden.
Sasa ana fursa ya kuweka rekodi ya mfungaji wa magoli mengi nchini
Ujerumani, ambapo kwa sasa anatoshana na Gerd Mueller wote wakiwa na
magoli 68.
Kiungo wa Bayern Bastian Schweinsteiger anahitaji kufanyiwa
upasuaji kwenye kifundo chake cha mguu.
Licha ya kukosekana kwa Schweinsteiger, Bayern wana
wachezaji sita kwenye orodha ya Löw wakiongozwa na nahodha Phillip Lahm.
Arsenal inawakilishwa na wachezaji wawili Mesut Ozil na Per
Mertesacker, huku pia Premier League ikiwakilishwa na mchezaji mwngine
kwa jina Andre Schuerrle wa Chelsea.
No comments:
Post a Comment