Rais
 wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi atafungua
 rasmi michuano ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 20 (U20) kwa 
klabu za Ligi Kuu ya Vodacom mwaka huu.
Uzinduzi
 wa mashindano hayo utafanyika kesho (Novemba 17 mwaka huu) kwenye 
Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam saa 2 kamili asubuhi. 
Mechi ya ufunguzi itakuwa ya kundi A kati ya Azam na Coastal Union. 
Mechi
 nyingine za kesho ni kundi; Yanga na Mbeya City (saa 8 mchana- Uwanja 
wa Karume), kundi B ni Ruvu Shooting na Ashanti United (saa 4 asubuhi- 
Uwanja wa Karume), Oljoro JKT na Simba (saa 10 jioni- Uwanja wa Karume).
Kundi
 C kutakuwa na mechi kati ya Kagera Sugar na Mtibwa Sugar itakayochezwa 
saa 2 kamili asubuhi kwenye Uwanja wa Azam Complex, na kwenye uwanja huo
 huo saa 10 jioni ni Rhino Rangers dhidi ya Tanzania Prisons.

No comments:
Post a Comment