KWA MAWASILIANO ZAIDI TUMIA BARUA PEPE rockersports212@yahoo.com AU TUPIGIE KUPITIA NAMBARI 0767166607 AU 0717166607. KARIBU SANA. 66666666607 AU 0717166607

Sunday, December 8, 2013

Licha ya zimwi wa vichapo kungangania kwa United, Moyes hababaiki

Meneja wa Manchester United, David Moyes bado anadhamiria kuongoza klabu hicho kutetea taji lao la Premier licha ya kichapo kingine mikononi mwa Newcastle Jumamosi.
Kiungo wa Ufaransa, Yohan Cabaye, alifunga bao la ushindi dakika ya 61 na kuwatuza Newcastle ushindi wa kwanza Old Trafford kwa miaka 41.
Janga hilo la kichapo lilifuatia kichapo cha awali cha bao 1-0 kutoka kwa Everton lakini Moyes bado anashikilia kwamba United wana uwezo wa kuhusika katika harakati za kunyakua taji la Uingereza.
"Matokeo yangekuwa bora," meneja huyo aliyekufa moyo huku vijana wake wakiendelea kumiliki nafasi ya tisa, alama 12 nyuma ya viongozi Arsenal.
"Tulihitaji bao ili kutupa imani lakini hatukubuni kikamilifu," aliongeza.
Alipoulizwa ikiwa United bado wamesalia katika kinyang'anyiro cha taji, Moyes alijibu, "Nasimama kidete kwamba tutakuwa karibu na ninatumahi tutakuwa miongoni mwa washiriki musimu ukikamilika."
Huku kurunzi ikimulikwa kwake tangu aridhi Sir Alex Ferguson, Moyes alikiri kwamba utawala mpya umekumbwa na mawimbu makali.
"Tumekosa mbinu za kufunga nyakati zinazofaa na tumeshindwa kutumia fursa ya kucheza pasi sawa. Tumepoteza mechi mbili 1-0 ambazo matokeo yalikuwa kinyume na mchezo."

No comments:

Post a Comment